Image
Image

ASASI YA YA SIASA, ULINZI NA USALAMA YA JUMUIYA YA MAENDELEO YA NCHI ZA KUSINI MWA AFRIKA SADC TROIKA YATAKIWA KUSIMAMIA MPANGO WA AMANI KATIKA KUTATUA MZOZO WA KISIASA WA MADAGASCAR.


                                  Jakaya Kikwete

Tanzania imekabidhi rasmi uenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (SADC-Troika) kwa Namibia, huku ikielezea mafanikio yaliyopatikana katika kushughulikia changamoto za kisiasa na usalama kwenye mataifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zimbabwe, Madagascar.

Mwenyekiti wa SADC - Troika aliyemaliza muda wake Rais Jakaya Kikwete, anayemaliza muda wake wa uongozi akizungumza nchini Malawi katika mkutano wa 33 wa wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini mwa Afrika SADC, ametoa taarifa ya utendaji katika kushughulikia mizozo ya kiasiasa miongoni mwa nchi wanachama ambapo ameitaka Namibia na nchi wanachama wa SADC kusimamia mpango wa amani na maagizo ya SADC, Umoja wa Afrika, umoja wa Mataifa katika kutatua mzozo wa uongozi Madagascar ili kuhakikisha yanatekelezwa kikamilifu kwa lengo la kumaliza mzozo wa kisiasa nchini humo.  

Rais Hifikepunye Pohamba, wa Jamhuri ya Namibia amepokea Uenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya nchi za kusini  mwa Afrika SADC-Troika kwa kipindi cha mwaak mmoja .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment