Faustine Shilogile.
Na.Jimmy Mengele,Morogoro.
Kamanda wa
polisi mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile amewaambia waandishi wa habari mjini
Morogoro kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na jeshi hilo kwa kushirikiana na
askari wa wanyamapori kutoka hifadhi ya taifa ya Udzungwa katika eneo Mzombe darajani
kata ya Kidodi barabara ya Ifakara
Mikumi baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema.
Amesema
watuhumiwa hao walikamtwa wakiwa kwenye gari lenye namba za usajili T 199
AQP Mitsubish Fuso lori ambalo lilikuwa
limepakia magunia ya mchele ambapo katika upekuzi, askari walifanikiwa kukuta
meno hayo yakiwa kwenye mfuko wa sandarusi(Sulphate) .
Mkuu wa
hifadhi ya taifa ya Udzungwa Nitalis
Uruka, pamoja na mkuu wa kikosi cha kuzuia ujangili kanda ya mashariki, wizara
ya maliasili na utalii Faustine Masalu wamezungumzia ujangili huo, pamoja na
kuwawasisitizia wananchi kukabiliana na vitendo hivyo vinavyoshika kasi nchini
vinavyoathiri maliasili ya taifa ambayo inapaswa kulindwa kwa maslahi ya
kizazi vya sasa na vijavyo.



0 comments:
Post a Comment