Image
Image

VITUO VITANO WILAYA YA KINONDONI VYAPOKEA MSAADA WA VITANDA 20 NA MAGODORO KWAAJILI YA AKINA MAMA WANAO JIFUNGUA.


                                                 Angela Kairuki.
Zahanati pamoja na vituo vya afya vitano katika wilaya ya Kinondoni jijini dar es Salaam vimepokea msaada wa vitanda 20 pamoja na magodoro wenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 50 kwa ajili ya akina mama wanaojifungua.
 
Msaada huo ni moja ya mikakati ya kukabiliana na upungufu wa vifaa tiba pamoja na vitanda kwa akinamama wazazi katika hospitali zilizokuwa chini ya halmashauri ya manispaa ya kinondoni.

Akikabidhi msaada huo katika moja ya zahanati iliyoko Kimara jijini dar es Salaam Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angela Kairuki amesema vifaa hivyo ni miongoni mwa mahitaji muhimu yanayotokana na ongezeko la wagonjwa pamoja na kuzijengea uwezo hospitali hizo ili kupunguza msongamano katika hospitali za mikoa.

Aidha kwa upande wake mganga Mkuu Mfawidhi katika zahanati ya kimara Dk.Alphonsina Mbinga amesema zahanati hiyo ambayo inahudumia kati ya wagonjwa 500-hadi 600  kwa siku inakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo upungufu wa watumishi pamoja na gari la wagonjwa .





Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment