Image
Image

SERIKALI KUPITIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI YAKAMILISHA UPIMAJI WA VIWANJA 35 KATIKA ENEO LA RWABASI LILILOPO BUHEMBA, WILAYA YA BUTIAMA MKOANI MARA KWA AJILI YA WACHIMBAJI WADOGO WA DHAHABU.



Augustine Mgendi, Mara.


Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini nchini imekamilisha upimaji wa Viwanja 35 katika eneo la Rwabasi lililopo Buhemba wilaya ya Butiama mkoani Mara kwa ajili ya wachimbaji wadogo wa Dhahabu.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa wilaya ya Butiama Bi Angelina Mabula Kufuatia kupatikana kwa Mwekezaji kutoka nchini Australia  ambapo amesema kukamilika kwa zoezi hilo ni kutokana na kauli ya Waziri wa Nishati na Madini  Prof Sospeter Muhongo katika hotuba yake ya Bajeti  kwa mwaka 2013/2014  iliyowahakikishia wachimbaji wadogo katika kata za Buhemba na Mirwa kutengewa eneo la uchimbaji wa Madini ya Dhahabu.

Amesema zoezi hilo limekuwa shirikishi kwa wachimbaji wa Maeneo hayo na hivyo kuwataka kuunda vikundi ili kupata Leseni zitakazowezesha kufanya shughuli za Uchimbaji katika Maeneo hayo.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amesema mbali na wachimbaji hao Wadogo kutengewa maeneo Uchimbaji lakini pia Wananchi wa eneo la Buhemba watanufaika na kuwepo kwa uwekezaji huo huku kamishina Msaidizi wa Madini kanda ya Ziwa akisema kuwa ofisi yake itafanya Mafunzo kwa wachimbaji wadogo mkoani Mara kuhusu utunzaji wa Mazingira,kujua sheria za Madini na ulipuaji wa miamba katika njia salama.

Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imempata Mwekezaji Kampuni Manjaro Resource kutoka nchini Australia ambapo itashirikiana na Kampuni ya STAMICO  kufanya Shughuli za Uchimbaji wa Madini katika Mgodi wa Buhemba uliopo wilaya ya  Butiama Mkoani Mara.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment