Image
Image

BUTIKU: VIONGOZI MSIPOKEE ZAWADI NA KUHALALISHA KWA KUZIPA JINA LA TAKRIMA.


                           Joseph Butiku

Viongozi nchini wametahadharishwa kuacha kupokea zawadi na kuzihalalisha kwa kuzipa jina la takrima.



Tahadhari hiyo ilitolewa na Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Joseph Butiku, alipokuwa akijibu swali la Mjumbe wa Baraza la Mabadiliko ya Katiba wilayani Handeni, Zawadi Chamosi.



Chamozi alitaka kupewa ufafanuzi kuhusu maana ya zawadi katika utumishi wa umma kwa mujibu wa ibara ya 15 kifungu kidogo cha kwanza.



Butiku alisema kuwa kiongozi akikubali kupewa zawadi anaweza hata kuuza siri za nchi kwani atalazimika kufuata matakwa ya aliyempa zawadi hiyo kama kulipa fadhila.



Hata hivyo alisema kitendo hicho ni kinyume na taratibu kwa mujibu wa sheria za kazi.
 
“Ningependa niwaambie kitu kimoja katika kifungu hiki, unaweza kupewa zawadi kutoka kwa wananchi kutokana na utendaji wako wa kazi, haikatazwi kwani kwa utaratibu kama ilivyoelezwa hapa zawadi hiyo ni zawadi ya Jamhuri ya Muungano," alisema.



Aidha alitolea ufafanuzi kuhusu hoja iliyotolewa na Diwani wa kata ya Kwamatuku, Mustafa Beleko, aliyekuwa mmoja wa wajumbe wa baraza hilo kuhusu  ibara ya 16 kifungu cha kwanza, ibara ndogo ya kwanza kifungu (b) kinachomtaka kiongozi wa umma kutangaza mali zake na za mwenzi wake na kwamba itahusu wake wote wa ndoa wa mhusika wanaotambulika kisheria.


 
“Hata kama ana wake wangapi ili mradi wanatambulika kisheria, atapaswa kutaja mali zao zote kwani wanashirikiana katika shughuli zao za kila siku, ni lazima mali na madeni yake yafahamike ili kujua idadi za mali zenu pamoja na watoto wenu wenye umri zaidi ya miaka kumi na nane,” alisisitiza.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment