Image
Image

JESHI LA POLISI MKOANI MWANZA LAKABILIANA NA WAFUASI WA CHADEMA KATIKA SHINIKIZO LA KUMG'OA MEYA WA MANISPAA YA ILEMELA JIJINI MWANZA:



Hawa ni askari wa jeshi la polisi mkoani mwanza wakiwa katika harakati za kuwatawanya wafuasi wa chama cha Democrasia na maendeleo chadema kufuatia kuibuka vurugu jijini humo.
Henry Kavirndo Mwanza. 

Jeshi la polisi mkoani Mwanza leo limelazimika kuwatawanya kwa mabomu ya machozi wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) baada ya kutaka kuandamana hadi katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo kumshinikiza kutoa majibu ya kutaka kumvua wadhifa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela mkoani humo Henry Matata na Naibu wake Swila Dede.
Suala jingine ambalo wafuasi wa chama hicho wanalihitaji ni kurejeshwa pia Madiwani watatu wa chama hicho waliovuliwa wadhifa huo.

Jeshi hilo limelazimika kuingilia kati maandamano hayo baada ya wafuasi wa chama hicho kufanya maandamano yaliyoanzia kata ya nyakato mkoani Mwanza na kuhitimishwa katika viwanja vya furahisha ambapo kwa mujibu wa duru za awali yalitarajiwa kupokewa na mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo ambaye hata hivyo hakuweza kufika uwanjani hapo.
Wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema wakionekana kubeba mabago kwa lengo la kudshinikiza 
baada ya kutaka kuandamana hadi katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo kumshinikiza kutoa majibu ya kutaka kumvua wadhifa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela mkoani humo.


Kutokana na mkuu huyo wa mkoa kutowasili uwanjani hapo kama ilivyotarajiwa kulingana na duru zilivyokuwa zimetanda mkoani hapa kwamba angeyapokea maandamano hayo wafuasi wa chama hicho ambao walikuwa wamekaa uwanjani hapo kwa muda mrefu wakimsubili mkuu huyo wa mkoa waliamua kuanzisha maandamano ya dharula ya kutaka kumfuata ofisini kwake.
Wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema wakionekana kubeba mabago kwa lengo la kudshinikiza 
baada ya kutaka kuandamana hadi katika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo kumshinikiza kutoa majibu ya kutaka kumvua wadhifa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilemela mkoani humo.

Katika vurugu hizo baadhi ya wakazi wa Jiji la Mwanza wakiwemo wafanyabiashara walijikuta wakilazimika kusitisha shughuli zao za kibiashara na wengine kuzikimbia ili kukwepa kudhurika na moshi wa mabomu ya machozi yaliyokuwa yakipigwa kuwatawanya wafuasi wa chadema.



Mtaa ukionekana kuwa safi kwa masaa machache baada ya askari hawa wa ffu kuwatawanya wafuasi hao.
Awali akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikilo amesema kuwa hawezi kulizungumzia suala hilo kwa kuwa linashughulikiwa kisheria.

Wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema waliwasha moto katika eneo hili, hapa askari wa kutuliza ghasia wakionekana kuondoa mawe baada ya kutuliza vurugu hizo jijini mwanza.


Wafuasi wa chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamelazimika kufanya maandamano hayo yaliyokuwa yakiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Ilemela Highnes Kiwia pamoja na Mbunge wa Jimbo la Nyamagana Ezekiah Wenje baada ya uchaguzi wa viongozi hao kupigwa kalenda tangu kikao cha kamati kuu ya Chama hicho Taifa kilipowavua uanachama ili kusubili maamuzi ya kisheria.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment