Image
Image

RAIS KIKWETE AVITAKA VYUO VIKUU KUONGEZA UDAHILI WA WANAFUNZI.



Rais Jakaya Kikwete, amevitaka Vyuo Vikuu na vyuo Vishiriki nchini kuongeza udahili wa wanafunzi, pamoja na kutoa shahada za uzamili na uzamivu kwa wingi ili kuongeza wakufunzi wengi watakaosaidia kuinua kiwango cha elimu nchini.



Kadhalika Rais Kikwete ameiagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuhakikisha wanatekeleza mpango wa kukuza elimu wa ‘matokeo makubwa sasa’ ili kuondokana na changamoto zinazozikabili nchi kwa sasa katika nyanja ya elimu.



Rais Kikwete alitoa maagizo hayo jana katika viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akitunuku hati Idhini kwa vyuo vikuu na vyuo vishiriki nane vya hapa nchini baada ya kuwa vimekamilisha taratibu zote za uanzishwaji wa chuo kikuu.



Alisema idadi ya wanafunzi wanaoingia katika vyuo vikuu kwa sasa haitoshi kulinganisha na udahili wa wanafunzi katika vyuo vingine vya nje.



kwa sasa idadi ya wanafunzi wanoingia vyuo vikuu ni 78,735 kwa mwaka ambayo inapaswa kuongezwa hadi kufikia 80,000.



Alisema kwa sasa vyuo vikuu na vishiriki vimeongezeka kutoka 37 awali hadi kufikia vyuo 52 kwa sasa.
Alifafanua kuwa Serikali imedhamiria kuiinua sekta ya elimu nchini, kwa kuongezea bajeti ya Wizara hiyo kutoka Sh. trilioni 2.1 kwa mwaka jana hadi kufikia Sh. trilioni 3.1 mwaka huu.



“Ongezeni idadi ya wakufunzi wenye sifa katika vyuo, pamoja na kuwezeka zaidi katika mafunzo ya uzamivu na uzamili hata mkiweza mkaazime wakufunzi nchi jirani,

” aisema Rais Kikwete.

Vyuo vilivyotunukiwa hati Idhini ni Tumaini Makumira (Tuma), Mtakatifu Augustino cha Tanzania (Saut), Kishiriki cha Ruaha (Ruco), Mount Meru (MMU), Arusha (UoA), Kishiriki cha Tumaini Dar es Salaam (Tumadarco),Taasisi ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia Arusha (NM-AIST), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (Must).



Naye Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema idadi ya wanafunzi wanaoingia vyuoni imeongezeka kutoka 1,39,638 kwa mwaka 2010/11 hadi kufikia 1,66,484 kwa mwaka 2011/12 sawa na asilimia 16.



Alisema katika kuboresha kiwango cha elimu, kuna wahadhiri 44 waliopelekwa Ujerumani kuongeza ujuzi.


Mwakilishi wa Mkuu wa Chuo cha Saut, Titus Mdoe alisema viongozi wa chuo wanatakiwa kuangalia mahitaji ya wanafunzi ili kuiinua elimu nchini.



Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri Tanzania, Dk. Alex Malasusa, alisema kutunukiwa kwa Idhini hiyo ni deni kubwa kwa wamiliki wa vyuo nchini kuhakikisha kiwango cha elimu kinakua.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment