Image
Image

UJENZI MPYA WA KITUO CHA MABASI YA MIKOANI MBIONI KUKAMILIKA.


       kurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe.

Kile kitendawili cha siku nyingi  lini kituo cha Mabasi yaendayo mikoani na nchi jirani kitaanza kujengwa katika eneo la Mbezi Luis kimeteguliwa baada ya Jiji kueleza kuwa ifkikapo Novemba mwaka huu kituo hicho kitaanza kujengwa.



Mwezi Januari mwaka huu, Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ilibomoa majengo yote yaliyokuwamo katika kituo cha Ubungo na kubakiza jengo moja la utawala, ikiwa ni maandalizi ya kuachia eneo hilo kwa ajili ya kujenga kituo cha mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam (Dart).



Baada ya Jiji kubomoa kituo hicho, lilikaa kimya bila kusema nini kinachoendelea huku likiahidi kwamba, kituo hicho kinachotumiwa na mabasi yaendayo mikoani kingehamishiwa Mbezi Luis.



Akizungumza kwa njia ya simu jana, Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe, alisema kuwa ujenzi wa kituo cha Mabasi yaendayo mikoani katika eneo la Mbezi Luis unatarajia kuanza Novemba mwaka huu baada ya kukamilika kwa taratibu mbalimbali.



Alisema kwa sasa mchakato wa kumtafuta mkandarasi atakayejenga kituo hicho unafanyika, na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi miwili kuanzia sasa.


Kabwe alisema kuwa ujenzi wa kituo hicho pindi utakapokamilika kitakuwa kituo kikubwa na cha kimataifa tofauti na kile cha awali cha eneo la Ubungo.



Aliongeza kuwa kituo hicho kitakuwa ni cha kudumu kwa kipindi kirefu kutoka kizazi hadi kizazi na hakitakuwa kituo cha muda au cha kuhama kwa miaka ya karibuni.



“Kitakuwa ni kituo kikubwa, unapozungumzia kituo cha mabasi yaendayo mikoani siyo kitu cha mchezo lazima tujipange kwelikweli kwa ujenzi, na hicho kituo kitakuwa ni cha miaka 70 ijayo,” alisema Kabwe.



Alisema kinachochelewesha kujengwa kwa kituo hicho kwa muda mrefu ni upatikanaji wa mkandarasi mwenye sifa na vigezo vya kujenga kituo, na kusema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam haikurupuki katika kutafuta mkandarasi, hivyo lazima utaratibu ufuatwe.



Kabwe alisema kuwa kwa sasa timu yake ya Jiji iko na washauri wataalam kwa ajili ya kuweka michoro ya ramani ya ujenzi wa kituo cha kisasa kitakacho chukua magari mengi.



Eneo la kituo cha mabasi ya mikoani Ubungo awali ilikuwa eneo la Shirika la Usafiri Dar es Salaam (UDA) kabla Serikali kubadilisha matumizi yake na kuwa kituo cha mabasi ya kwenda mikoani na nchi jirani.

Hata hivyo  serikali hiyo hiyo imebadilisha  matumizi ya kituo cha mabasi ya mikoani na kuwa kituo cha magari ya mwendo kasi DART mradi unaotarajia kukamilika mwaka 2014.



DART WAZUNGUMZIA UJENZI WA KITUO NA KARAKANA ENEO LA UBUNGO

 Kwa upande wake, mradi wa mabasi yaendayo haraka (Dart)  walipotafutwa ili kueleza ni lini ujenzi wa kituo na karakana utaanza kujengwa baada ya wafanyabiashara wote kuondolewa, mtaalamu mshauri mawasiliano wa Dart, Jack Meena alisema kazi ya ujenzi ilishindikana kuanza mapema kutokana na kukosekana kwa fedha za kulipia fidia kwa waathirika wa ujenzi. 



Alisema  sababu nyingine ni katika kipindi ambacho mkandandarasi alitakiwa aanze ujenzi kulitokea mafuriko ambayo yalizuia kuanza kwa ujenzi ( Mvua zilizonyesha mwaka 2011). 


Sababu nyingine Meena alisema  ni kufunguliwa kwa kesi mahakamani na wafidiwa.

Kutokana na kesi hizo kulikuwa na zuio la mahakama kusitisha ujenzi mpaka kesi zitakapomalizika

Hata hivyo, alisema Serikali ipokatika mchakato wa kushirikisha sekta binafsi katika ujenzi wa vituo vya mabasi yaendayo mikoani kupitia sera ya Public Private Partnership (PPP), na kusema kuwa kwa sasa bado mabasi hayo yataendelea kufanya shughuli zake katika kituo cha Ubungo mpaka hapo miundombinu itakapojengwa na kukamilika.



TANROADS  WAZUNGUMZIA UJENZI WA VITUO VYA DALADALA

Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) walipoulizwa ujenzi wa vituo vya daladala kwa ajili ya mabasi ya Dart utakamilika lini, Mtendaji Mkuu wa Tanroads, Mhandisi Patrick Mfugale alijibu kuwa miundombinu na vituo vinatarajiwa kukamilika Machi, 2015 endapo hapatakuwa na ucheleweshwaji wowote katika utekelezaji wa mikataba ya ujenzi wa miundombinu hiyo.



Alipoulizwa sababu gani zinazosababisha kutoanza kujengwa kwa karakana ya mabasi ya mradi wa Dart katika eneo la Ubungo wakati ubomoaji wa vibanda vilivyokuwapo katika eneo hilo ulifanyika muda mrefu.

Aliongeza kwa kusema kuwa Tanroads inaendelea kufanya mazungumzo na wadau kupitia na kuridhia mapitio ya usanifu ujenzi utaanza mara moja.



“Awali ujenzi wa karakana ulitarajiwa kukamilika ndani ya miaka miwili, lakini kutokana na kupungua kwa kazi baada ya kuhamishwa kwa kituo cha mabasi yaendayo mkoani, ujenzi utachukua kati muda wa mwaka mmoja hadi mwaka mmoja na nusu,” alisema Mfugale
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment