Image
Image

WANAJESHI WA JWTZ TANZANIA WAELEKEA NCHINI ANGOLA KUSHIRIKI MAZOEZI YA KIJESHI.



Wanajeshi 35 kutoka jeshi la ulinzi la wananchi wa TANZANIA,JWTZ,wameondoka jana kuelekea nchini ANGOLA,kushiriki mazoezi ya kijeshi ya pamoja kwa nchi za SADC yanayotarajiwa kufanyika nchini humo kuanzia leo na kuhusisha vikosi vya anga pekee.

Akizungumza na wanajeshi hao kabla hawajapanda ndege, mkuu wa vikosi makao makuu ya Jeshi, Meja Jenerali HASSAN CHEMA, amewakumbusha wanajeshi hao kuzingatia nidhamu ya hali ya juu kwenye ushiriki wao na kuhakikisha sifa ya majeshi ya Tanzania katika weledi na uadilifu vinaendelea.

Amesema mazoezi hayo yajulikanayo kama BLUE ZAMBEZI 2013 yanafanyika kwa mara ya nne sasa, ambapo tanzania imekuwa ikishiriki mara zote likiwamo zoezi lililojulikana kama BLUE RUVUMA ambalo limewahi kufanyika hapa nchini katika mikoa ya LINDI na MTWARA.

Awali akisoma taarifa kabla ya kukagua na kupitisha gwaride rasmi la askari hao, mkurugenzi wa ufundi makao makuu ya jeshi, BRIGADIER GENERALI OMARI MATEKA, alisema wamejiandaa kikamilifu kushiriki zoezi hilo na kuahidi kuonesha uzoefu walionao katika kukabiliana na majanga mbalimbali.

Wanajeshi hao kabla ya kupanda ndege ya jeshi kuelekea Angola walifanya gwaride fupi na kutoa heshima zao kwa mgeni rasmi  meja jenerali Hassan Chema ambaye mara tu baada ya gwaride alikabidhi bendera ya TANZANIA kwa kiongozi wa msafara huo ambae ni brigadier generali Matteka na kisha kuwapa mkono wa kwaheri.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment