Image
Image

TUME YA MABADILIKO YA KATIBA YATAKIWA KUTUPILIA MBALI MAWAZO YANAYO TOLEWA NA BARAZA LA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU ZANZIBAR.



Tume ya mabadiliko ya katiba imetakiwa kuyatupilia mbali mapendekezo ya rasimu ya mabadiliko ya katiba yatakayotolewa na Baraza la Wanafunzi wa Vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu Zanzibar, baada ya kuzuiliwa kwa wajumbe kutoka vyuo vikuu viwili visiwani humo.

Jumla ya vyuo vikuu 11 kati ya 13 vilivyopo Zanzibar vinawakilishwa na wajumbe 106, lakini wajumbe 47 ndio wanaoshiriki katika mchakato huo, huku wajumbe 20 wa Baraza la katiba kutoka Chuo kikuu cha Zanzibar na Chuo cha Maendeleo ya Utalii wakitimuliwa baada ya kupinga msimamo wa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar kuhusu Muungano.

Wakizungumza na Tambarare Halisi katika kampasi ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar kilichopo Beitrasi, wanafunzi waliofukuzwa wamesema endapo tume itapokea maoni hayo itakuwa haijawatendea haki wanafunzi wa Vyuo vikuu ambao wamekosa kutoa yao kutokana na kufukuzwa kwa wawakilishi wao.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Wanafunzi wa vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu Zanzibar, Juma Kombo Hamad amesema wajumbe wa baraza hilo wamefikia uamuzi wa kuwafukuza kutokana na kitendo chao cha kususia kikao na kutangaza kujiondoa katika mchakato huo.




Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment