Khamis Suleiman, Dar es Salaam.
Jeshi la Polisi kanda maalum Dar es salaam limefanikiwa kuokoa
shilingi millioni 15 kati ya shilingi millioni 28 zilizoporwa na majambazi
wawili kwa mfanyabiashara William Mathias eneo la Buguruni malapa jijini Dar es
salaam.
Kamishna wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam CP Suleiman
Kova akizungumza na waandishi wa habari amesema majambazi hao wakiwa na silaha
walimvamia mfanyabiashara huyo baada ya kumfuatilia na baadae kumtishia kwa
silaha na kumpora fedha hizo.
Mara baada ya uporaji wananchi pamoja na waendesha bodaboda
walianza kuwafukuza ambapo majambazi hao walitumia mbinu ya kurusha fedha ili
watoroke lakini walidhibitiwa na polisi waliokuwapo eneo hilo.
Aidha katika kupambana na madawa ya kulevya jeshi hilo
limefanikiwa kukamata shehena ya madawa ya kulevya aina ya bangi yakiwa katika
mabegi makubwa kumi, na mapipa matano pamoja na kuwashikilia watuhumiwa 231,
ambapo pia imekamata mtandao wa wezi wa vioo vya magari, na vioo vya magari
zaidi ya elfu moja.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi linawashikilia wafanyakazi
wawili wa shirika la umeme tanesco kwa wizi wa Transfoma mbili kutoka katika
ghala la tanesco lililopo kinondoni jijini dsm.
0 comments:
Post a Comment