Image
Image

KATIBU WA JUMUIYA NA TAASISI ZA DINI YA KIISLAM SHEIKH PONDA ISSA PONDA AFIKISHWA MAHAMANI MJINI MOROGORO NA KUSOMEWA MASHITAKA UCHOCHEZI:


 Shekh Ponda Issa Ponda aliyevaa shati nyekundi akiwa katika  mahakama ya hakimu mkazi mkoani Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili dhidi yake.
Jimmy Mengele Morogoro.
Katibu wa jumuiya na taasisi za kiislamu nchini Shekh Ponda Issa Ponda amesafirishwa kwa na helkopta ya jeshi la polisi  katika mahakama ya hakimu mkazi mkoani Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili ambayo ni kutotii amri halali, kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini na kushawishi kutenda kosa kinyume na mashariti ya kifungo cha nje alichohukumiwa na mahakama ya hakimu mkazi ya Kisutu.
Hili ni gari la polisi ambalo lilikuwa linahakikisha kwamba ulinzi unaimarika katika mahakama ya hakimu mkazi mkoani morogoro alikokuwa Sheikh ponda issa ponda  akisomewa mashitaka matatu yaliyokuwa yakimkabili dhidi yake leo hii.

Shehe Ponda akiwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi amewasili mkoani Morogoro akitokea jijini Dar es Salaam kwa lengo la kusomewa mashitaka katika mahakama ya hakimu mkazi mkoani Morogoro majira ya saa tano asubuhi kwa helkopta ya jeshi la polisi.
Hii ni helkopta ya jeshi la polisi iliyokuwa imembeba katibu wa jumuiya na taasisi za kiislamu nchini sheikh ponda issa ponda kwa kusomewa mashitaka yanayo mkabili katika mahakama ya Hakimu mkazi mkoani morogoro.
Akisomewa mashitaka hayo akiwa amekaa kutokana na kudai kuwa na maumivu ya jeraha kwenye bega, wakili mkuu wa serikali kanda ya Morogoro Benard Kongola amedai kuwa Shekh ponda anatuhumiwa kutenda makosa hayo matatu Agosti 10 mwaka huu majira ya jioni katika viwanja vya shule ya msingi kiwanja cha ndege Manispaa ya Morogoro.
Shekh Ponda Issa Ponda aliyevaa shati nyekundi akiwa katika  Ndege kwenye mahakama ya hakimu mkazi mkoani Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili dhidi yake huku jeshi la polisi likionekana imara kweli kweli.
Katika shitaka la kwanza la Shekhe Ponda anadaiwa kutotii amri halali ambapo shitaka la pili anadaiwa kutoa maneno yenye nia ya kuharibu imani za dini kwa kutoa maneno ambayo yamenukuliwa yakisema ìSerikali iliamua kupeleka jeshi Mtwara kushughulikia suala la vurugu zilizotokana na gesi kwa kuwaua na kuwatesa wananchi kwa sababu asilimia 90 ya wakazi wa Mtwara ni waislamu kitendo ambacho ni kosa la jinai kifungu 129.

Shitaka la tatu linalomkabili Shekh Ponda ni kushawishi na kutenda kosa ambapo anadaiwa kutoa maneno ya ushawishi kwa waislam kutokubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za misikiti akidai zinaundwa na BAKWATA ambao ni vibaraka wa CCM na serikali.

Baada ya kusomewa mashitaka hayo Sheikh Ponda anayetetewa na mawakili Barthoromew Tarimo na Ignas Punge, amekana mashitaka yote na hivyo upande wa mashitaka kupinga dhamana kwa madai kuwa Shekh Ponda anatumikia kifungo cha nje na kwamba hakutakiwa kufanya kosa.
Shekh Ponda Issa Ponda aliyevaa shati nyekundi akiwa akiwa chini ya ulinzi wa jeshi la polisi  katika  mahakama ya hakimu mkazi mkoani Morogoro kujibu mashitaka matatu yanayomkabili dhidi yake.
Aidha upande huo wa mashitaka umedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika, hivyo mshitakiwa atarudishwa mahakamani Agosti 28 mwaka huu kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali ya mashitaka yanayomkabili na kwa sasa amerejeshwa rumande.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment