Image
Image

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAPENDEKEZA: URAIA WA NCHI MBILI UWE WA HAKI YA KIKATIBA.




Sekretarieti ya Baraza la Katiba la wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa limependekeza uraia wa nchi mbili uwe haki ya kikatiba kama zilivyohaki nyingine huku ikitaka muungano wa serikali mbili uendelee na mapungufu yafanyiwe marekebisho.

Aidha Baraza hilo limependekeza kuwa katika sera ya mambo ya nje ambayo inajumuisha uteuzi wa mabalozi, Rais baada ya kuteua mabalozi bunge kupitia kamati inayoshughulikia mambo ya nje uteuzi huo uidhinishwe na taasisi hiyo ya umma.

Akiongea na wanahabari mara baada ya ufunguzi wa kikao cha baraza hilo la mchakato wa katiba mpya,mwenyekiti wa baraza hilo,Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa BERNARD MEMBE ametoa rai kwa asasi, taasisi na makundi ya watu walioruhusiwa na tume ya mabadiliko ya katiba kisheria watumie fursa hiyo kukusanya maoni kwa jamii badala ya kufanya mikutano ya hadhara.

Baraza hilo lililowajumuisha watumishi mbalimbali waandamizi wa wizara hiyowakiwemo wastaafu katika ngazi ya uwaziri na mabalozi wa Tanzania katika nchi mbalimbali ambapo mjumbe wa Tume ya mabadiliko ya katiba,Dk,SALIM AHMED SALIM ameyasisitiza mabaraza kusaidia marekebisho yaliyomo katika rasimu ya katiba mpya ili kutengeneza katiba ya wananchi na sio ya kikundi fulani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment