Image
Image

ASILIMIA KUMI NCHINI KENYA YATENGWA KUKUZA KILIMO CHA NAZI




Serikali ya Kenya kupitia wizara ya kilimo imetenga shilingi milioni 500 kupiga jeki kilimo cha nazi katika mkoa wa pwani. 

Waziri wa kilimo nchini Kenya Felix Koskei, anasema serikali imejitolea kukuza zao hilo kwa sababu lina uwezo wa kuipa Kenya pato la shilingi bilioni 25 kila mwaka. 

Serikali ya Kenya imekuwa ikitoa shilingi milioni 80 kila mwaka kutumika kukuza zao hilo lakini waziri Koskei anasema ili kukuza zao hilo ipasavyo inabidi fedha hizo kuongezwa. 

Kwa sasa zao hilo linaipa Kenya mapato ya shilingi bilioni 6.2 kila mwaka kutoka shilingi bilioni 3.2 miaka ya hapo awali. 

Waziri huyo alisema serikali imepania  kukuza sekta hiyo ya kilimo cha nazi kwa asilimia 10 kila mwaka.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment