Image
Image

JESHI LA KENYA LIMEWAUWA WAPIGANAJI SITA WALIOKUWAPO KWENYE JENGO LA MADUKA MJINI NAIROBI KENYA




Kituo cha televisheni cha Citizen nchini Kenya kimeripoti kuwa, vikosi vya ulinzi vya Kenya vimewaua wapiganaji sita waliokuwa bado kwenye jengo la maduka mjini Nairobi.

 Awali, serikali ya Kenya ilisema kuwa kuna wapiganaji kati ya 10 na 15 ndani ya jengo la maduka ambamo watu 62 wameuawa na wengine 175 kujeruhiwa. 
Mapigano mapya yalizuka asubuhi ya leo na kuvunja hali ya ukimya iliyodumu usiku kucha iliyoashiria kumalizika kwa mapigano kati ya vikosi vya usalama vya Kenya na wapiganaji wa kundi la Al Shabaab. 

Ofisa mmoja wa polisi ambaye hakutaka kutaja jina mara moja amesema, vikosi vya usalama vinafanya msako katika jengo hilo ili kuhakikisha kuwa hakuna maguruneti au vifaa vyovyote vya kulipuka ambavyo vimeachwa na magaidi hao. 

Ameongeza kuwa, watu hawataruhusiwa kuingia ndani ya jengo hilo kwa muda kwa kuwa bado kuna miili ya watu ndani ya jengo hilo ambayo haijatolewa. 

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya anatarajiwa kulihubiria taifa baadaye leo. 

Kundi la Al Shabaab la Somalia limekiri kuhusika na shambulizi hilo na kusema, limefanya hivyo ili kulipiza kisasi kutokana na hatua ya serikali ya Kenya kupeleka jeshi lake kusini mwa Somalia kupambana na wapiganaji wa kundi hilo.

Shambulizi hilo ni kubwa zaidi kutokea nchini humo baada ya lile la mwaka 1998 ambapo ubalozi wa Marekani nchini Kenya ulishambuliwa na wapiganaji wa kundi la Al Shabaab la Somalia na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 200.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment