Image
Image

UCHUKUZI WA ANGANI NCHINI RWANDA KUCHANGIA UKUAJI WA UCHUMI NCHINI HUMO.



Mamlaka ya uchukuzi wa angani nchini Rwanda imetangaza kuwa inatarajia sekta hiyo kuchangia pakubwa katika ukuaji wa uchumi nchini humo. 

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka hio Daktari Richard Masozera akiongea na gazeti moja la kila siku nchini humo amesema sekta hiyo inakua kwa haraka jinsi ilivyokusudiwa. 

Masozera anaeleza kuwa ukuaji wa sekta hiyo lazima utachochea kuboreka kwa uchumi sambamba na sekta zingine muhimu za kibiashara nchini. 

Mamlaka hio inaeleza kuongezeka kwa idadi ya abiria na pia mashirika yanayotumia viwanja vya ndege nchini humo ni ishara ya mamlaka hiyo inachangia kukua kwa uchumi nchini humo. 

Idadi ya abiria wanoatumia anga nchini humo imeongezeka kutoka 280,000 hadi 500,000 katika muda wa miaka 5 pekee.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment