Image
Image

WATU 78 WAMEUAWA KATIKA MASHAMBULIZI PAKISTAN NA WENGINE 146 KUJERUHIWA



Serikali ya Pakistan imesema watu wasiopungua 78 wameuawa na wengine 146 kujeruhiwa katika mashambulizi ya mabomu yaliyotoke katika kanisa moja mjini Peshawar, kaskazini magharibi mwa Pakistan. 

Msemaji wa hospitali ya huko amesema, waliouawa ni pamoja na askari wawili, watoto 7, na wanawake 34, na idadi ya vifo huenda ikaongezeka kwa kuwa baadhi ya majeruhi wako mahututi. 

Baada ya mashambulizi hayo kutokea, waumini wengi wakristo walifanya maandamano katika miji mbalimbali nchini Pakistan, wakiitaka serikali ihakikishe usalama wa makanisa nchini humo.
Rais Mamnoon Hussein wa Pakistan na waziri mkuu Bw. Nawaz Sharif walilaani vikali mashambulizi hayo. 

Habari nyingine zinasema kundi la Taliban nchini Pakistan limetangaza kuwajibika na mashambulizi hayo, na kusema wataendelea kuwashambulia watu wasio waumini wa dini ya kiislamu, hadi ndege za Marekani zisizo na marubani zitakaposimamisha mashambulizi katika sehemu ya kaskazini magharibi mwa Pakistan.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment