Mmoja wa maskauti akiteremka kutoka juu ya mti
wakati mafunzo ya siku nne ya maskauti wilayani mpanda wiki ya Maadhimisho ya
Vijana na Kumbukumbu ya Mwalimu ya miaka 14 bila ya baba wa Taifa, mwalimu
Nyerere. Lakini maskauti hao bado wanamuenzi kwa kukumbuka kwa kukumbuka yale mazuri aliyoyaacha ikiwemo
kuwa na uzalendo kwa Taifa na moyo wa
ujasiri kitu ambacho kimeanza kupotea miongoni wa mwa watanzania walio wengi
hasa kizazi cha sasa.
Kamishina
wa SKAUTI Jonas Clavery akiwa na Katibu Tawala Wilaya ya Mpanda Donald Nkoswe
wakati akikagua moja ya kazi zilizofanywa na maskauti wakati wakiwa kwenye
mafunzo ikiwa ni sehemu ya mafunzo yao katika maeneo ya kambi baadaya ukaguzi
huo wa kazi alifanya shughuli ya kukabidhi vyeti kwa wahitimu hao wa mafunzo ya awali ya skauti yaliyohusisha
walimu wa shule za Msingi na Sekondari wapatao 50 mkoani humo.
..........................................................................................
Ismael Mohamed (Bin majid).
Vijana wa skauti katika mkoani wa Katavi jana wameadhimisha siku ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kwa kuenzi mambo yake
aliyokuwa akiyapendelea ya uadilifu moyo wa huruma, kujituma na kuthamini
uzalendo wa taifa kwa kuonesha kwa vitendo yale mambo mwalimu aliyokuwa akiyafanya na kuyapenda enzi za uhai wake sambamba na uadilifu, uzalendo.
Changamoto hiyo ilitolewa na Makamishina wa Skauti Mkoa wa Katavi Jonas Clevery wakati akimkaribisha Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima wakati wa kufunga mafunzo ya awali ya Skauti kwa walimu wapatao 50 wa Shule za Msingi na Sekondari yaliyochukua muda wa siku nne kuwafunza ukakamavu na maadili ili wakafundishe mashuleni kwao watoto maadili mema.
Katika
maadhimisho hayo maskauti hao wa Mkoani Katavi wakiongozwa na Kamishina wa
Skauti Mkoani humo Clavery Jonasi alieleza kuwa wameamua kuweka kambi ya
maskauti nje ya Mji ili kuweza kuwapatia mafunzo ya Skauti walimu wa Shule za
Msingi na Sekondari ili waweze kuelewa vizuri
umuhimu wa mafunzo ya Skauti kwa Jamii kuwa yanajenga moyo wa uzalendo
kwa kuwajenga vijana hasa walioko mashuleni na vyuoni, moyo wa ujasiri, wakizalendo wa kuipenda nchi na kuondoa migomo ya mara kwa mara inayojitokeza kwa
baadhi ya wanafunzi shuleni na vyuo hapa
nchini.
Kamishina
huyo alieleeza kuwa Watanzania wengi maadili yamepungua ikiwemo uzalendo tofauti na wakati wa enzi za mwalimu.
Amesema kuwa sasa hivi watu wamekuwa hawana uzalendo mawazo yao makubwa wana penda Rushwa, uchochezi wa migomo na kupandikiza chuki isiyo na tija kwa taifa.
Kwa kuliona
hilo wao kama skauti wameamua kuanzisha mafunzo ya skauti kwa walimu wa shule
za msingi na sekondari ili nao
wakafundishe wanafunzi wao mashuleni kwa kuwajengea uzalendo kwa kuanza
kuwafundisha kuwajengea uzalendo na kuipenda nchi kwa kuwapa mafunzo ya
ukakamavu, uzalendo na ujasili hali ambayo itasaidia kuwajenga zaidi
tofauti na wakati huu ambapo mambo yanaenda ndivyo sivyo.
Awali
akisoma risala miongoni mwa wahitimu wa mafunzo
ya awali ya Skauti Lucy
Mzunda alieleza kuwa miongoni mwa changamoto
walizokabiliana nazo katika
mafunzo yao ni pamoja na ukata kwa kukosa posho ya kushiriki katika mafunzo
hayo kwa kuwa wao ni watumishi wa umma walimu walipashwa kulipwa posho ya siku
nne kuka nje ya kituo cha kazi lakini bado hawajalipwa wanaoba kulipwa.
Changamoto
nyingine ni eneo la kuweka kambi
ambalo wameomba kukabidhiwa wamilikishwe
liwe mali ya skauti ya kuwa wanaweka kambi ili waweze kulitunza na kuwa endelevu kwa ajili ya kuhifadhi mazingira yasiharibiwe kwa kuwa wao ni skauti
watali tunza na kulihifadhi.
Akiongea na
wahitimu wa Mafunzo hayo kwa niaba ya Mkuu wa
Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima Katibu Tawala wa Wilaya ya Mpanda Donald
Nkoswe, amewataka wahitimu wazingatie yale yote waliyojifunza na waende wakawafundishe uzalendo wanafunzi
wao ili waweze kuwa wazalendo wa kupenda nchi yao
Aidha
ameaahidi kushughulikia madai yao yote waliyo yatoa na kuyafanyia kazi kwa
kuyafikisha katika eneo husika ili yaweze kufanyiwa kazi,katika hatua nyingine
kutokana na kugushwa na mafunzo hayo ameahidi kuchangia shilingi laki moja ili
kusaidia katika mafunzo ya jayo awamu nyingine ya mafunzo.
Wahitimu hao wametunukiwa vyeti vya kuhitimu
mafunzo, na umahili katika stadi mbalimbali za kujifunza ikiwemo ukakamavu,
uadilifu,taaluma na maigizo katika mafunzo hayo ambayo yamefana sana nakuonesha umahili wa hali ya juu kwa
wahitimu waliopata mafunzo kutoka kwa wakufunzi wao.
Wakati wa kufunga mafunzo hayo ya siku nne yakiambata na wiki ya Vijana na maazimisho ya kumbukumbu ya kifo cha mwalimu NyerereChangamoto imetolewa kwa watanzania kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa Vitendo ili kuendana na matendo ili kuenzi yale yote aliyokuwa akiyafanya wakati wa Utawala wake.



0 comments:
Post a Comment