Image
Image

VIKOSI VYA MISRI VYA INGILIA KATI MAPIGANO YA WAFUASI WA MORSI.




Vikosi vya usalama vya Misri vimelazimika kuingilia kati baada ya kuzuka mapigano kati ya wafuasi na wapinzani wa Mohamed Morsi Rais halali wa nchi hiyo aliyepinduliwa na jeshi huko Mansoura katika kaunti ya Dakhlia. 

Mapigano hayo yalitokea jana wakati pande mbili hizo zilizokuwa kwenye maandamano tafauti katika Chuo Kikuu cha al Mansoura kuanza kurushiana mawe. 

Polisi wa kutuliza ghasia waliingilia kati mapigano ya wapinzani na wafuasi wa Morsi kwa kuwanyunyizia gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya.

Hata hivyo hadi sasa hakuna ripoti iliyotolewa juu ya watu waliouawa au kujeruhiwa kwenye ghasia hizo huko Mansoura.

Misri imekuwa ikishuhudia ghasia na mapigano kati ya wafuasi na wapinzani wa Morsi katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo tangu kupinduliwa na jeshi, rais huyo halali mwezi Julai mwaka huu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment