Image
Image

UNIC NA YUNA WATEMBELEA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI KWENYE VYUO MBALI MBALI JIJINI ARUSHA.

Wajumbe wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) na wawakilishi wa Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA/UNCTN) wakiwa kwenye mazungumzo ya awali na Mkuu wa Shule ya Arusha (Madam Kitigwa) baada ya kuwasili katika shule hiyo kwa lengo la kukutana na Kilabu cha Umoja wa Mataifa shuleni hapo na kuzungumza na Wanafunzi kuhusiana na agenda mbalimbali za Umoja huo. 

Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa kikishirikiana na Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa (YUNA) wapo katika ziara ya kuzitembelea shule zenye na zisizo na Vilabu vya Umoja huo kwa lengo la kufikisha habari na kazi za Umoja wa Mataifa.

Afisa Habari wa Kituo cha Umoja Mataifa (UNIC) Bi. Usia Nkhoma Ledama akizungumza na wanafunzi-wananchama wa klabu ya Umoja wa Mataifa katika Shule ya Msingi Arusha Medium ambapo amewasisitiza juu ya umuhimu wa kuzifahamu agenda mbalimbali za Umoja Mataifa na nafasi yao katika kuleta maendeleo chanya kwa jamii.
Mwenyekiti Taifa wa Vilabu vya Umoja wa Mataifa Tanzania Bara na Visiwani (UNCTN) Bw. Rahim Rajab Nasser akizungumza na vijana wa shule ya msingi Arusha Medium juu ya umuhimu wa vilabu hivyo na umuhimu wa ushiriki wao kuanzia shule za msingi mpaka Sekondari na Vyuoni.
 Afisa Habari wa Kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa Bi. Usia Nkhoma Ledama (katikati) akisisitiza jambo kwa vijana wa shule ya msingi Arusha Medium. Kulia ni Mkutubi wa Maktaba ya kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) Bi. Harriet Macha na kushoto Mwenyekiti Taifa wa Vilabu vya Umoja wa Mataifa Tanzania Bara na Visiwani (UNCTN) Bw. Rahim Rajab Nasser.
Kobe mwenye umri sawa na shule ya Msingi Arusha Medium iliyojengwa mwaka 1930 akiwa hai mpaka na kuwa kivutio kwa wageni mbalimbali wanaofika shuleni hapo ikiwemo Wajumbe wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) na wawakilishi wa Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA/UNCTN).
Pichani juu na chini ni baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Arusha waliobahatika kushiriki mkutano huo ulioendeshwa na Wajumbe wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) na wawakilishi wa Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA/UNCTN).


 Wajumbe wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) na wawakilishi wa Asasi ya Vijana wa Umoja wa Mataifa (YUNA/UNCTN) wakiwa na mwenyeji wa msafara wao MC Kalinga wa Arusha wakielekea kukutana na wanafunzi wa Usa-River Academy


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment