Image
Image

RAIS BARACK OBAMA NA VIONGOZI WENGINE WAMZUNGUMZIA MAREHEMU MZEE MANDELA ENZI ZA UHAI WAKE.



Viongozi mbalimbali duniani wanaendelea kutuma salamu zao za rambirambi kufuatia kifo cha rais wa zamani wa Afrika Kusini Mzee Nelson Mandela.

Katika salamu zake za rambirambi, rais barack Obama wa Marekani amesema Mzee Mandela aliibadilisha Afrika Kusini na kuuendesha ulimwengu na alipata mafanikio mengi zaidi kuliko mtu mwingine yeyote na kuongeza kwamba dunia imepoteza mmoja wa watu wenye ushawishi na ujasiri.

Mjini London, waziri mkuu wa Uingereza bw. David Cameron ametuma salamu za rambirambi kwa kusema Mzee Mandela ni miongoni mwa watu walioing'arisha zaidi dunia na kwamba hakuwa tu shujaa wa kipindi kilichopita bali ataendelea kuwa shujaa wakati wote.

Kansela wa Ujeruani Angela Merkel amesema Mzee Mandela ni mfano wa ubinadamu ambaye sifa yake itawapa moyo watu ulimwenguni kote huku katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon akimuelezea Mzee Mandela kama bingwa wa haki duniani.
Rais wa zamani wa Marekani Bill Clinton, ambaye alikuwa madarakani Nelson Mandela alipochukua urais nchini Afrika Kusini, ameomboleza kifo cha shujaa huyo kwa kusema alikuwa "bingwa wa hadhi ya binadamu na uhuru".
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment