Image
Image

Yafahamu mambo mazito yaliyokuwa yakijadiliwa leo Bungeni



Licha ya kuwa na mambo mengi lakini mkutano wa 18 wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambao umeanza leo tarehe 27 January  mjini Dodoma pamoja na mambo mengine ilikuwa kwanza ni kuapishwa kwa Mwanasheria Mkuu mpya wa serikali Bwana GEORGE MASAJU na kujadiliwa na kupitishwa kwa miswada mitatu ya sheria.
Kipindi cha maswali na majibu:
Swali- Ezeckiel wenje
: Kuhusu makazi ya walimu.
Majibu- Naibu waziri: Mahitaji ya nyumba ni kmakubwa, serikali inajiandaa kufanya ukarabati, Walimu wanatakiwa kuishi kwenye nyumba za serikali bila kutozwa kodi
Majibu ya swali la nyongeza: Walimu wanapaswa kuishi kwenye nyumba za serikali bure.
Swali- Zitto Kabwe: Anauliza kuhusu fedha wanazokatwa walimu kwaajili ya makazi.
Majibu- Naibu waziri: Swala la watumishi kukatwa fedha lilitokana na kanuni za utumishi ambazo zilirekebishwa, na sasa walimu waliokatwa wanatakiwa kurejeshewa fedha zao.
Majibu- Waziri : Ni kweli bado shule binafsi zinaenda kinyume na maagizo ya serikali, Shule zisizotekeleza taratibu za serikali zitafutwa.
Swali- Dk Dhakifu: Wazazi hawana uwezo wa kulipa ada, Lini serikali itatamka kutoa elimu ya bure.
Majibu - Waziri: Serikali imeadhimia kila mtoto anapata elimu ya msingi na sekondary na Mheshimiwa raisi ametangaza adhma ya serikali ya kutoa elimu ya sekondary.
Ahmedi mwidau Swali- Uhaba wa walimu kwenye shule za serikali
Majibu- Waziri wa elimu: Wizara imeanzisha mafunzo ya stashada ya juu ya masomo ya uwalimu. Serikali inamkakati wa kuendelea kuajiri walimu wa sayansi na hisabati, imeajiri mwaka jana na mwaka huu itaajiri walimu wengine. Serikali inamkakati wa kukarabati vyuo vya uwalimu.
Swali la nyongeza:
Majibu- Waziri: Vivutio kwa walimu wa Hesabu na Sayansi, Serikali inapenda kuweka vivutio kwa walimu wote hususan walimu wa sayansi na hesabu, Serikali inajiandaa kuboresha Mishahara na mazingira ya kufundishia.
Kuhusu TEHAMA na umeme katika shule, Kwenye miradi ya umeme almashauri zimeelekezwa kufikisha umeme kwenye mashule.
Swali- Mh Msola: Chuo cha sanaa cha Mkwawa, kwanini kisitumike kufundisha masomo ya Sayansi pekee badala ya kuwa chuo cha sanaa kama ilivyo hivi sasa ?
Majibu- waziri: Wazo la proffesa ni zuri na serikali ipo karika mchakato wa kulitekeleza hilo. na sasa inaboresha maabara ya chuo hicho.
WIZARA YA MAWASILIANO:

Swali Mh Mwanausi: Ni lini wananchi wa mpakani mwa Tanzania na msumbiji watapatiwa mawasiliano.
Majibu: Maeneo ya mpakani na maeneo yake yamewekewa mpango maalumu na kufikia July mwaka huu yatakuwa yamepatiwa mawasiliano.
Note: Wabunge wanapouliza maswali Sauti inakata kwahiyo inakuwa kazi kupata maswali yanayoulizwa na pia majibu yanashindwa kueleweka.
Kwenye majibu ya nyongeza: Kampuni ya simu ya VIATEL itakuwa kampuni yenye ubora wa hali ya juu kwasababu inaanza na mtandao wa 3g moja kwa moja tofauti na makampuni mengine.
WIZARA YA NISHATI NA MADINI
Swali la nyongeza- Mh Mangungu:

Majibu- Naibu Waziri : Sio kwamba serikali inachukuwa muda mrefu lakini mahitaji yamekuwa mengi. Sio kwa
mba kila eneo la kijijini linatoza hizo pesa, kinacholipwa elfu 27 ni VAT tu, maeneo ambayo mradi wa lea haujafika wananchi wanaendelea kulipa.
Swali- la Mh Magdalena Hamisi Sakaya: ikuhusu mradi wa REA.
Majibu: Jumla ya vijiji 41 vipo kwenye mpango wa REA. Mradi unawaunganisha wateja 1550, kazi inaendelea na utekelezaji umefikia zaidi ya asilimia 50. mradi unatarajiwa kukamilika mwaka 2015.
Swali la nyongeza- Mh Masudi:
Majibu: Wananchi wa kaliua watapata umeme, kuandaa mipando na kuagiza vifaa inachukuwa muda mrefu sana, lakini vifaa vikifika utekelezaji unachukuwa muda mfupi.
Swali- Mh kapuya: Naishukuru sana wizara ya nishati na madini kwa kufikisha umeme kwenye kijiji cha Kawira.
WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
Swali: 
kuhusu Shilingi m250 zilizotengwa kwa ajili ya kukarabati majengo ya wazee .
Majibu naibu waziri wa Afya: 
Wizara inafanya tathmini ili kuangalia jinsi ya kuboresha zaidi makazi ya wazee
Swali la nyongeza: Makazi ya Kiilima ni mabovu sana nyumba hazina madirisha wala milango, hakuna vyoo wala chakula cha uhakika, Waziri anasema kunampango wa kufanya ushirikiano na DANIDA, saa ni lini serikali itakamilisha mpango huo. Je kunampango gani wa kutoa chakula cha uhakika kwa wa
zee hao.
Majibu- Naibu waziri: Katika mwaka unaokuja wa fedaha serikali itaingiza vituo hivi kwenye bajeti kwa awamu . Serikali inampango wa kupunguza makazi haya ili kuongeza udhibiti.
Swali la nyongeza - Mh Rweikiza: wazee wanaishi kwa kutegemea wafadhili, kwanini serikali iseweke bajeti kwa ajili yao
Majibu: 
Wafadhili wanaojitokeza ni walioguswa na sio njia kuu ya kuwatunza wazee hao, serikali inatenga bajeti
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
Swali- Rajabu Mbaruku Mohammed: Tatizo la tembo kuzaliwa bila meno serikali inachukua hatua gani ?
Majibu: Tembo wote huzaliwa bila meno lakini meno huota baadaye, kuna taarifa za kuongezeka kwa tembo wasiokuwa na meno, seriali inafanya utafiti ambao umelenga kuthibitisha taarifa hizi, utafiti huu haukuwa wa kina na haukulenga kuleta ufumbuzi.
Swali la nyongeza :
Majibu : Ni kweli nilikiri kwenye vyombo vya habari kuwa Idadi ya tembo wasiokuwa na meno inaongezeka na sababu ni kwamba tembo wasiokuwa na meno sio waathirika wakubwa wa ujangili.
Swali- Mh Mbatia:
Jibu: Ni kweli wizara ya maliasili inachangia 19% kwenye pato la taifa na tunampango wa kuongeza mpaka a
silimia 30, bado tunahimiza utalii wa ndani.
WIZARA YA UJENZI
Swali- Bwanausi: kuhusu baranara ya masasi na daraja la ukama.
Majibu- Naibu waziri wa Ujenzi : Serikali imekubali na imejicomit kukamilisha ujenzi wa barabara hii, kuhusu daraja serikali italifatilia kuona kitu gani inaweza kufanya.
Swali la nyongeza la Mh Mkapa:
Majibu: Ujenzi wa daraja unaendelea kuhusu ukamilifu wake serikali itamfatilia mkandarasi ili kuhakikisha kazi hiyo inafanyika kwa ufanisi na wakati.
Swali la nyongeza- Dk Chami:
Majibu- Naibu waziri wa ujenzi: Ni kweli swala hili lipo ndani ya ilani ya chama cha mapinduzi na kazi hii imeshafanyika kwa awamu. Tunapozungumzia ujenzi wa barabara inajumuisha na daraja.
WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
Swali- Mh Mashishanga (Viti maalumu): Kuhusu kiwanda cha kusindika nyama Shinyanga kilichokuwa kinamilikiwa na Tanganyia Pekas
Majibu- Naibu waziri: Kampuni inayosimamia ipokwenye mchakato wa kutafuta mbia mwingine atakaewekeza kwenye mitambo mizuri zaidi ya kuchinja na kusindika nyama.
Majibu ya swali la nyongeza: Sasa tufike mahali tusaidiane tutafute mbia mwingine.
Swali- Mch Mwanjari: Hata mbeya kuna kiwanda hakifanyi kazi serikali inasema nini juu ya swala hili.
Majibu: Hili nalo tunaliunganisha na jibu lililotangulia.
WIZARA YA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
Swali- Kwanini serikali isiondoe kodi kwenye mashirika ya kidini
Jibu- Naibu waziri: Kodi ambayo mashirika haya yanatozwa ni tsh 8000 ambayo ni kiasi kidogo sana ukilinganisha na kodi zinazotozwa kwenye asasi zingine, hivyo serikali haina mpango wa kuondoa kodi hiyo kwa sasa ili mashirika hayo yachangie hata kidogo.
Swali lanyongeza- Mh Ragge: Serikali inatoa kauli gani kwa manispaa zinazotoza kodi zaidi ya tsh 8000?
Majibu - Naibu Waziri: Serikali inakemea vikali Manispaa zote zinazotoza zaidi kinyume na maagizo ya serikali.
Matangazo
Mswada wa Twakimu unaondolewa kwenye orodha ya shughuri za bunge, Serikali inataka kuurekebisha zaidi. Mswada wa kodi
Mh Wenje: 
amesimama lakini Sauti imekatika.
Spika anasitisha shughuri za bunge hadi Kesho saa tatu Asubuhi.
Cdt.J.F
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment