Image
Image

Afcon 2015: DRC yajiandaa kuweza kumenyana na Cote d'Ivoire

Leo ni siku ya maandalizi ya timu za taifa za soka za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Cote d'Ivoire kujiandaa kwa mchuano wa nusu fainali, kuwania taji la ubingwa wa Afrika.

Mechi hiyo itachezwa Jumatano Februari 4 katika uwanja wa Bata nchini Equatorial Guinea kuanzia saa nne usiku saa za Afrika Maashariki sawa na saa tatu usiku saa za Afrika ya Kati.

Mataifa haya mawili yalimenyana mwaka uliopita katika mechi ya kufuzu kucheza fainali hizi, DRC walifungwa mabao 2 kwa 1 nyumbani na walipokwenda Abidjan waliwafunga Cote d'Ivoire mabao 4 kwa 3.

Hii ni wazi kuwa mechi haitakuwa rahisi Jumatano wiki hii, na kocha wa Leopard Florent Ibenge atakuwa anataka kudhirihisha kuwa ana uwezo wa kuiongoza timu yake kufika fainali, sawa na Mfaransa Herve Renard ambaye lengo lake ni kuhakikisha kuwa Cote d'Ivoire inanyakua taji hilo walilonyakua mwisho mwaka 1992.

Nusu fainali ya pili itakuwa siku ya Alhamisi kati ya Ghana na wenyeji Equatorial Guinea katika uwanja wa Malabo.
Mshambualiaji wa Ghana, As
amoah Gyan anauguza jeraha.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment