Image
Image

Kaya masikini zapongeza uanzishwaji wa mpango wa TASAF awamu ya tatu Singida

Waziri wa nchi ofisi ya rais mahusiano na uratibu Dk.MARY NAGU akizungumza na Wananchi wa Singida hawapo pichani.
Baadhi ya kaya maskini mkoani SINGIDA zimepongeza serikali kwa kuanzisha mpango wa tasaf awamu ya tatu ambao umesaidia kupunguza hali ngumu ya maisha kwa kuziwezesha kaya hizo kupata mahitaji muhimu ikiwa ni pamoja na kugharamia ada na uniform za watoto wao.
Wametoa kauli hiyo kwa waziri wa nchi ofisi ya rais mahusiano na uratibu , MARY NAGU wakati alipotembelea kaya zinazonufaika na mradi huo ambapo kwa mkoa wa SINGIDA zaidi ya kaya elfu 42 zinanufaika na mpango huo.
Mpango huo wa tasaf awamu ya tatu ulizinduliwa mwezi agosti mwaka 2012 na Rais Jakaya kikwete na miaka miwili baadae mkoa wa SINGIDA uliunganishwa rasmi katika mpango huo ambao mpaka sasa zaidi ya shilingi bilioni tatu zimekwishatumika .
Takwimu zinaonyesha kuwa Mkoa wa SINGIDA unakaya zaidi ya laki 240 zenye kiwango kikubwa cha umaskini .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment