Image
Image

Msigwa:Rais ajaye awe na upeo wa kuliongoza taifa ili liondokane na ukata wa umasikini unao likabili



WAZIRI Kivuli wa Maliasili na Utalii ambaye pia ni Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), amesema Watanzania wanahitaji rais ajaye awe na malengo,upeo wa kutatua changamoto ili taifa liondokane na umaskini.

Mchungaji Msigwa aliyasema hayo wakati akihojiwa kwenye Kipindi cha Dakika 45 kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha ITV na kusisitiza rais ajaye lazima awe na uwezo wa kifedha si maskini ili asiwafanye Watanzania waendelee kuwa maskini.

Alisema kama ni tajiri, awaeleze Watanzania utajiri wake ameupata wapi isiwe umetokana na fedha za wizi na kutaka wagombea wote wapimwe akili na uwezo wao wa kuongoza wananchi.

"Rais ajaye awe na uwezo wa kukabiliana na wimbi la umaskini linalowatesa Watanzania wengi, achambue mambo na kuwapeleka Watanzania katika njia inayoleta mafanikio," alisema.

Aliongeza kuwa, lazima kiongozi anayefaa kuwa rais apimwe akili na afya ili wananchi wafahamu ndipo achaguliwe na akipita aanze kuwatumikia Watanzania akiwa na afya njema.

Aliwataka wananchi wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika vyama vya siasa kama ubunge, udiwani na urais ili taifa liweze kupata viongozi bora.

Mchugaji Msigwa alisema wale wanaosema rais ajaye anapaswa kuwa kijana hicho si kigezo kinachohitajika ili kumpata kiongozi bali awe wa umri wowote ila mwenye uwezo wa kuchanganua mambo na mwenye dira ya kuona mbele.

Alisema Chama Cha Mapinduzi (CCM), kikiendelea kubaki madarakani mwaka huu ni majanga; hivyo umefika wakati wa Watanzania kufanya mabadiliko.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment