Image
Image

Shirika la AMNESTY lazitupia lawama serikali kwa kushindwa kulinda raia wake dhidi ya mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola

Shirika la haki za binaadamu la Amnesty International limezilaumu serikali ulimwenguni kwa kushindwa kuwalinda mamilioni ya raia dhidi mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola na makundi yenye silaha.
Ripoti ya mwaka ya shirika hilo imezielezea hatua ambazo zimechukuliwa na ulimwengu dhidi ya migogoro nchini Nigeria na Syria kuwa ni za kutia aibu.
Ripoti hiyo imeyalaumu mataifa tajiri duniani kwa kutumia nguvu na fedha nyingi kuwazuia watu kuingia kwenye mataifa hayo, kuliko kuwasaidia watu kuishi.
Amnesty International imeuelezea mwaka 2014 kuwa uliokuwa na mauaji mengi zaidi yaliyofanywa na vyombo vya dola na makundi ya waasi katika nchi zaidi ya 35 duniani, zikiwemo Jamhuri ya Afrika ya Kati na India.
Ripoti hiyo inatabiri kuwa kutakuwa na mauaji na ghasia zaidi katika mwaka huu, kutokana na kusambaa na kupata nguvu kwa makundi kama Boko Haram na Islamic state -IS.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment