Jeshi la Polisi Mkoani KAGERA limefanikiwa kuzima jaribio la utekaji wa
magari katika eneo la NYAKANAZI wilayani BIHARAMULO,na kukamata bunduki
NNE aina ya SMG, Risasi MIA MOJA NA ISHIRINI NA TISA pamoja na sare za
jeshi la nchi moja jirani.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa KAGERA ACP HENRY MWAIBAMBE amesema
baada ya mapambano ya kurushiana risasi na watu hao wanaosadikiwa kuwa
majambazi katika pori la NYANTAKARA kwa takribani dakika KUMI,
majambazi hao walitokomea mahala kusikojulikana.
Baadhi ya vitu mbalimbali vilivyonaswa na Jeshi la Polisi mkoani
KAGERA ambavyo ni pamoja na bunduki NNE aina ya SMG,risasi mia moja na
ishirini na tisa , MAGAZINE SITA ,pamoja na sare za nchi jirani.
Aidha katika hatua nyingine Kamanda MWAIBAMBE amewashukuru wananchi
wa kijiji cha Kabale kata ya NYAMAHANGA wilayani BIHARAMULO kwa kusaidia
kukamatwa kwa majambazi wawili ambao walikutwa na furushi lililokuwa na
nyenzo mbalimbali zinazosaidia kutekeleza uhalifu.
Home
News
Jeshi la Polisi mkoani kagera lazima jaribio la utekaji magari katika eneo la NYAKANAZI wilayani BIHARAMULO
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment