Image
Image

Maonyesho ya miradi ya kibiashara kufanyika Dar

Ushindani wa biashara unaozidi kukua kila siku umepelekea Kampuni ya East Afrika Unique (TIPEC), kubuni na kupanga maonyesho ya kukuza uwekezaji kwa wafanyabiashara wa hapa nchini ili kuweka msukumo zaidi kwenye uwekezaji.
Maonyesho hayo yatakayofanyika jijini hapa Juni mwaka huu, yatatanguliwa na semina kwa wafanyabishara mbalimbali ili kuwajengea uwezo wa kubuni mradi mikubwa itakayoweza kupata wawekezaji.

Mkurugenzi Mtendaji wa TIPEC Rodgers Mbaga aliwaambia waandishi habari leo kuwa, wamefikia hatua hiyo baada ya kuona kwamba wafanyabishara wengi wanafikiria kuwa na miradi midogo wakati zipo fursa nyingi zaidi katika miradi mikubwa.

Alisema, maonyesho hayo ambayo yatafanyika kwa mara ya kwanza jijini hapa yanalenga wafanyabishara  wenye miradi isiyopungua dola za Kimarekani 250,000 sawa na Sh 500 milioni za Kitanzania.

“Tunataka wafanyabiashara wetu na wamiliki wa miradi mikubwa, kufikiria kuwa na ndoto kubwa ili waweze kupata mafanikio makubwa lakini pia kuwavutia wawekezaji wanaopenda kuwekeza kwenye miradi mikubwa,”alisema Mbaga na kuongeza kuwa hakuta kuwa na kuuza bidhaa.

Alisema, kabla ya maonyesho hayo wafanyabishara binafsi na wataasisi binafsi watapewa semina inayolenga kuwajengea uwezo wa kutayarisha miradi ambayo itawavutia wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi kwenye maonyesho hayo.

Ofisa Mwandamizi Ukuzaji Masoko wa kampuni hiyo, Stephen Koberou, alisema maonyesho hayo yatasadia wafanyabishara kupata wawekezaji kwenye miradi yao.

“Lakini ikifika kwenye utekelezaji fursa nyingine kama ajira zitaongezeka, uzalishaji wa biadhaa zitakazokuwa zinauzwa  ndani na nje ya nchi utaongezeka,”alisema Koberou na kuongeza hayo yote ni mchango katika kukuza  uchumi wa nchi.

Naye, Mwakilishi kutoka Baraza la Taifa la Biashara, Victoria Hingira alisema, watahakikisha kuwa wanashirikiana na TIPEC ili miradi ya wafanyabiashara iweze wawekezaji.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment