Image
Image

Amiri jeshi mkuu Rais kikwete aongoza mazishi ya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya kyerwa luteni kanali Benedict kitenga (MSTAAFU) mkoani morogoro.


Rais Jakaya Kikwete ameongoza mamia ya wakazi wa mkoa wa Morogoro  katika mazishi  ya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Kyerwa Luten Kanali mstaafu Benedict Kitenga  aliezikwa  kijeshi   katika makaburi ya kola mjini morogoro. 
Akizungumza na waombolezaji nyumbani kwa marehemu Kola Hill mkoani Morogoro Rais Kikwete amesema serikali imepoteza kiongozi muhimu aliekuwa mchapakazi    ambapo amewataka ndugu na wanafamilia kuwa na moyo wa uvumilivu hasa katika wakati huu mgumu wa kuomboleza kifo cha ndugu yao.
Akitoa salamu kwa niaba ya  mkuu wa majeshi  majeshi Device Mwamunyange  Meja  Jenerali Nerali  Salum Kijuu amesema marehemu alilitumikia jeshi la wananchi JWTZ kwa uadilifu na uaminifu  huku  mwenykiti wa wakuu wa wilaya nchini Jason Msome umoja wa wakuu wa wilaya  wamestusha na kifo hicho ambapo wameeleza maerhemu alifanya kazi zake kwa ushirikiano wa karibu na wenzake hadi umauti ulipo mkuta.
Kwa upande wake ndugu wa marehemu wameshukuru serikali kwa jitihada za kumuuguza marehemu  na kuiomba serikali kuendelea kuwa karibu na familia ya marehemu katika masuala mbalimbali hasa katika wakati huu mgumu wa maombolezo huku askofu mkuu wa jimbo la morogoro Telesphol Mkude amewataka watanzania kufanya matendo yanayompendeza mwenyezimungu kwani hapa duniani tutaondoka na uzima wa milele upo mbinguni.
Marehemu benedict kitenga amefariki april 20 katika  hospitali ya taifa ya muhimbili na kuzikwa pril 23 katika makaburi ya kola mjini morogoro ambapo mazishi yake yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa  chama na serikali   akiwemo waziri mkuu mizengo pinda ,waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu tawala za mikoa na serikali za mitaa hawa ghasia na waziri wa nchi ofisi ya rais utumishi selina kombani wakumuu wa mikoa na wakuu w awilaya .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment