Image
Image

Waziri Chiza ahudhuria kongamano Kubwa la Biashara Visiwa vya Comoro

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu( Uwekezaji na Uwezeshaji) Mhe. Mhandisi Christopher Chiza (Mb) akibadilishana mawasiliano na baadhi ya wafanyabiashara waliowasili Visiwa vya Comoro kwa ajili ya kushiriki katika Kongamano la BIashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Comoro, linalotarajiwa kufanyika tarehe 23 Aprili, 2015. Kulia (mwenye miwani) ni Balozi wa Tanzania Visiwa vya Comoro Bw. Chabaka Kilumanga. 
Na.Mwandishi wetu Comoro.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Mhe. Mhandisi Christopher Chiza (Mb) ahudhuria Kongamano Kubwa la Biashara kati ya Comoro na Tanzania, litakalofanyika tarehe 23 Aprili, 2015 Visiwani Comoro.

Lengo kuu la kongamano hilo ni “kuongeza kiwango cha biashara na uwekezaji kati ya Tanzania na Comoro kwa kutambua fursa zilizopo kati ya nchi hizi mbili na kurasimisha biashara ambayo kwa sasa hairatibiwi”.
Kongamano hilo ambalo litawakutanisha viongozi, maafisa wandamizi wenye dhamana ya kuendeleza biashara kutoka Tanzania na Comoro pamoja na wadau wa Sekta Binafsi, litafungua rasmi fursa ya kutangaza na kuuza bidhaa zinazozalishwa Tanzania kwa wafanyabiashara watakaopenda kufanya hivyo kutokana na nafasi nyingi za biashara na uwekezaji zilizopo katika Visiwa vya Comoro.

Miongoni mwa mada ambazo zitazungumzwa katika kongamano hilo ni pamoja na; Mada kadhaa kuhusu fursa za biashara na uwekezaji nchini Tanzania na Comoro, mazingira ya biashara za uwekezaji nchini Tanzania na Comoro, fursa zinazopatikana katika nchi hizo na usaidizi wa kiserikali katika kurahisisha baishara. Aidha, itakuwapo fursa ya mazungumzo ya kina kati ya wafanyabiasha wa Comoro na Tanzania (business to business discussions).

Aidha, zipo fursa nyingi za uwekezaji katika uzalishaji na usindikaji wa bidhaa za kilimo, pamoja uwekezaji katika sekta ya huduma za afya, elimu, mawasiliano na nishati endapo fursa hizi zitatangazwa na kuwekwa miundombinu ya uhakika ya usafiri kati ya Tanzania na Comoro bidhaa za Tanzania zitapata soko la uhakika visiwani Comoro.  
Kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na wafanyabiashara na wadau mbalimbali  kutoka Tanzania, limeandaliwa na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania nchini Comoro, kwa kushirikiana na kampuni ya 361 degrees ya Dar es Salaam. Kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Mamlaka ya Uendelezaji wa Biashara Tanzania (TANTRADE) ambao wanahamasisha na kuwakaribisha wafanyabiashara wa Tanzania, Exim Bank, Shirika la Ndege la Air Tanzania, Jumuiya ya Wafanyabiashara Wenye Viwanda na Wakulima ya Comoro (UCCIA); na Mamlaka ya Kuendeleza Vitega uchumi vya Comoro (INM).
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment