Mshindi wa mwezi wa shindano la twitte Harrykageyo akikabidhiwazawadi mara baada ya kuibukamshindi wa shindano la 3N.co.tzMachi2015 na kuzawadiwa Tsh 10milion leo April 15,2015.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr.Reginald Mengi amesema
Watanzania wanaweza kuondokana na umaskini iwapo mawazo na fikra sahihi
zitatumika kuwawezesha wananchi wake kutumia raslimali za asili kujikwamua
kiuchumi.
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi
ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa hafla ya kuwatangaza na
kuwazawadia washindi wa mwezi wa Marchi wa shindano la twitte wazo la biashara
alilolianzisha ili kuwahamasisha watanzania kujikomboa kiuchumi.
Mshindi wa kwanza kwa mwezi Marchi aliyezawadiwa
ruzuku ya shilingi milioni 10 ni mhitimu wa elimu ya Kompyuta wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Bukary Kibonajoro, aliyebuni wazo la
kutengeneza Program ya kompyuta ya kusimamia biashara za wafanyabiashara wadogo.
Washindi wengine 9 ambao mawazo yao yaliingia katika
10 bora walizawadiwa shilingi milioni moja kila mmoja.Hao ni pamoja na Salim
Said, Harry Kageyo,Abdallah Mdira,Victor Byemelwa, na Norman Billy. Wengine ni Atumilikye
IsaacStephen Maswe, Irene Enock na Joyce Patrick Tano.
Mapema Mkuu wa jopo la majaji Dr. Donath Ulomi, na
Jaji mwenzake Dr. Jabu Mwasha walisema
mwezi uliopita idadi ya Twitter zilizopokelewa na kushindanishwa zilikuwa ni
nyingi kuliko miezi iliyopita, na kutoa ushauri wa namna bora ya kubuni wazo
bora.
0 comments:
Post a Comment