Image
Image

Katoni za maji ya kunywa kutoka kampuni mbali mbali zilizoingizwa kinyemela kutoka nchini Kenya zakamatwa na kuteketezwa.


Jumla  ya katoni 574 ya maji ya kunywa kutoka kampuni mbalimbali nchini kenya yenye thamani ya shilingi milioni 3,444,000 ambayo yadaiwa kuingizwa nchini kinyemela na bila kuthibitishwa na mamlaka ya chakula na dawa TFDA na vibali wala   nembo  ya shirika la viwango nchini (TBS)  yakamatwa na  kuteketezwa.

Akizunguza wakati wa zoezi la uteketezaji wa maji hayo ambao umefanyika katika eneo la nyabange  nje kidogo ya  manispaa ya musoma, meneja  msaidizi usimamiaji madeni na kodi za ndani wa TRA Bw Ernest Nkangaza,amesema kuwa maji hayo ya aina mbalimbali kutoka nchi hiyo jirani,yameingizwa nchini kwa njia za panya kati ya machi 9 na april 9 mwaka huu,na kusambazwa katika miji ya tarime na Musoma.

Naye afisa afya mkoa wa mara Bw.Bumija Mhando,amesema maji hayo kiafya si mazuri kwani  yamegunduliwa kuwa ni maji ya kisima,ambayo ukaguzi wake haufahamiki na hivyo usalama wake  unatia mashaka makubwa huku yakiwa na bei ndogo ukilinganisha na makampuni mengini.

Zoezi hilo la uteketezaji limefanywa na mamlaka ya mapato tanzania TRA Mkoa na idara ya afya  likisimamiwa na maafisa kutoka jeshi la polisi na usalama wa taifa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment