Miili iliyotambuliwa ime chukuliwa na ndugu zao tayari kwa maziko
na mwili mmoja ambao bado haujatambuliwa umehifadhiwa katika Hospitali
ya Wilaya ya Kahama kwa siku saba na baada ya hapo utazikwa na Serikali.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Wilaya ya Kahama,BENSON MWAMPESYA,hadi
sasa hakuna miili mingine
iliyopatikana licha ya msaada wa mitambo ya kuchimba eneo hilo na
wataalamu kutoka katika machimbo ya Bulyanhulu
ambao tayari wameshaanza kazi hiyo
kwa siku ya tatu leo .
Amesema kazi inakuwa ngumu
kutokana na mvua kubwa zinazoendelea
kunyesha na m ashimo hayo yana
kina kirefu hivyo zoezi hilo linachukua muda hadi kufika katika eneo lililokuwa
na wachimbaji hao chini ya ardhi.
0 comments:
Post a Comment