Timu ya viongozi wa chama ACT wazalendo ikiongozwa na
kiongozi wao mkuu,Zitto Kabwewapo katika ziara ya siku mbili mkoani
singida kwa ajili ya kukijenga na kukiimarisha chama hicho kipya.
Akizungumza mwenyekiti wa ACT wazalendo mkoani singida Wilfred Kitundu,
kwenye timu hiyo yupo pia mwenyekiti wa taifa Anna Mghwira na katibu
mkuu,Samson Mwigamba.amedai kuwa maandalizi yote muhimu kwa ajili ya ziara
hiyo,yamekamilika.
Akifafanua juu ya ziara hiyo,Kitundu amesema kuwa ziara hiyoiliyoanza siku ya leo juma tano asubuhi itafungua matawi
yao mapya katika kijiji cha kintiku na mawili mjini manyoni na baadaye ofisi ya
kanda mjini singida.
Amesema baada ya kumaliza ziara wilayani manyoni, mchana atakwenda
wilaya ya singida mjini ambapo atafungua matawi matatu ya chama hicho katika
kijiji cha kisaki, utemini, na ukombozi na pia ofisi ya kanda.
Kitundu amesema baada ya kumalizika kwa ziara hiyo jimbo la Singida
mjini,kesho yake aprili kumina sita,msafara huo utahamia wilayani
iramba ambapo utafungua matawi ya ulemo, misigiri na sokoni kiomboi,
kisha kuendelea na ziara yake mkoani shinyanga.
Mwenyekiti kitundu
amewaomba wakazi wa mkoa wa Singida kujitokeza kwa wingi kumpokea na
kumsikiliza zitto kabwe katika maeneo atakayopita na kuhutubia
juu ya itikadi, falsafa na misingi ya chama hicho.
0 comments:
Post a Comment