Image
Image

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kampala (KIU) kilichopo Gongo la mboto wafunga bara bara wakishinikiza kusajiliwa kwa kozi zote za sayansi na bodi husika


Wanafunzi wa Kitivo cha Sayansi ya Afya Chuo Kikuu cha Kampala (KIU)  kilichopo  maeneo ya Gongo la mboto wilaya ya ilala  jijini Dar es Salaam  wamegoma kwa kufunga barabara katika  lango kuu la chuo hicho kuuzuia uongozi kuingia au kutoka hadi malalamiko yao yatakapopatiwa ufumbuzi wa kudumu ambao umekuwa ukifanya kutokea migomo ya mara kwa mara chuoni hapo.
 Wanafunzi hao wameshinikiza uwepo wa  waziri mwenye dhamana ya Elimu nchini tanzania Bwa. Shukuru kawambwa na waziri Mkuu Mizengo Pinda kufika chuoni hapo  kusikiliza kilio kinacho wakabili kwa katika Upande wa Afya kutokana na ungozi ndani ya chuo kushindwa kusikiliza kwa wakati na kulitolea ufafanuzi wea kudumu.
Wakati wa maandamano zilikuwa zikisikika sauti na nyimbo zenye shinikizo la kutaka kiliochao kisikilizwe kwa wakati huku wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe mbali mbali yakutaka popote alipo waziri mwenye dhamana na mkuu wake kufika na kusikiliza kile kinacho wakabili katika upande wa Afya.
Kufuatia mgomo huo ulililazimu jeshi la polisi kufika eneo hilo ili kuweza kutuliza ghasia na mambo mengine ambayo yanaweza kutokea na kuhatarisha hali ya usalama,ambapo jeshi la polisi liliwaamuru weanafunzi hao waliokuwa wakiandamana kutawanyika mara moja katika eneo hilo kabla haijatumika nguvu ya ziada ambayo ingeweza kuchafua hali ya hewa kwa muda mfupui.
Kwa mujibu wa wanafunzi hao, tangu waanze mgomo Aprili 10 mwaka huu, uongozi wa chuo hicho haujataka kuwasikiliza.
Wakizungumza  na TAMBARARE HALISI wanafunzi wa chuo hicho waliainisha madai takriban saba wakidai ni ya muda mrefu ambayo hayajapatiwa suluhu.
“Tumegoma kwa sababu kwanza kozi zote za sayansi hazijasajiliwa na bodi husika na watu waliohitimu wamenyimwa leseni za kazi,” alisema mmoja wa wanafunzi wa mwaka wa pili wa Shahada ya Famasia,alisema wanalipa ada kubwa ikilinganishwa na wanafunzi wa mwaka wa kwanza.
“Wanafunzi wa mwaka wa pili na wa tatu wanalipa kuanzia Sh milioni 6.5 hadi Sh milioni tisa na kwa mwaka wa kwanza wanalipa Sh milioni tatu,” alisema mwanafunzi huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake.
Madai mengine ya wanafunzi hao ni pamoja na kutokuwa na mtaala unaoeleweka, uongozi mbovu akiwamo mshauri wa wanafunzi, programu kuchukua miaka mingi tofauti na vyuo vingine, kushindishwa mitihani kwa makusudi na gharama kubwa ya kurudia mitihani waliyoshindwa.
Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano, Kenneth Uki, alikiri kuwapo madai hayo ingawa mengine si ya kweli,alisema kuhusu kozi kutosajiliwa na bodi husika, alisema ni kweli Bodi ya Famasia haijasajili kozi za famasia huku ingawa alisema si kweli kwamba kozi zote za sayansi hazijasajiliwa.
“Tulishapeleka maombi Bodi ya Famasia tangu 2013 na walikuja kufanya ukaguzi awamu ya kwanza na bado hawajarudi kwa awamu ya pili na ya tatu waweze kutupatia usajili,” alisema Uki.
Akizungumzia ada,Uki alisema tayari yamekwisha kupokewa maombi ya wanafunzi kupunguziwa ada na kwamba kikao cha bodi ya chuo huwa ni mara moja kwa mwaka hivyo wavute subira.
“Ada ni mkataba kati ya chuo na wanafunzi kwa hiyo linapokuja suala la kutaka ipungie ni suala la makubaliano baada ya wanafunzi kupeleka maombi yao  yanaweza yakakubaliwa au kukataliwa, ” alisema Uki.
Hata hivyo alisema wanafunzi wanapochagua chuo hawana budi wasome masharti ya chuo husika ikiwamo ada na kozi zinazotolewa.
Kuhusu madai ya kushindishwa mitihani wanafunzi na gharama kubwa za kurudia mitihani, alisema wanafunzi wamekuwa watoro na kwamba inahitaji fedha kufanya maandalizi ya kurudia mitihani.
Msajili wa Baraza la Wafamasia katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Elizabeth Shekalaghe amekiri kuwapo maombi ya usajili kutoka KIU akisema bado zinasubiriwa baadhi ya nyaraka kutoka chuoni hapo.l
“Tulipokea maombi kutoka KIU tukaenda kufanya ukaguzi chuoni hapo na kuwapa masharti na vigezo walivyotakiwa wakamilishe pamoja na kuleta nyaraka, hawakuleta.
“Tukawakumbusha mara mbili Agosti na Septemba mwaka jana bado hawakufanya hivyo ,”alisema Shekalaghe.
Alisema sheria inavitaka vyuo husika visajili kwanza kozi zao na ndipo vifanye udahili wa wanafunzi na kila baada ya miaka mitatu vinatakiwa kukaguliwa upya.
Migomo nchini tanzania na kwingineko imekuwa ikifanyika kwa lengo la kutaka kusikilizwa kwa kile wanachotaka kisikike kutokana na mamlaka husika kushindwa kulipatia suluhu hivyo kuamua kupaza sauti kwa umoja na mshikamano ili pengine kila anayesikia huenda akaguswa na hivyo utatuzi ukapatikana kwa wakati unaostahili.
Licha ya kuaminika kuwa sauti ya pamoja ionayovuma kwa lengo la kudai haki kwa maandamano lakini pia sauti hiyo hiyo kama haijatumika vema kwa misingi ya sheria na kanuni zake huenda ikaleta madhara kama ambayo yaliyowahi kutokea katika maandamano kadhaa ya watu kuumizwa,kupoteza masha na hata wengine kubakia na ulemavu wa kudumu katika viungo vya miili yao.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment