Wanafunzi
hao wameshinikiza uwepo wa waziri mwenye dhamana ya Elimu nchini
tanzania Bwa. Shukuru kawambwa na waziri Mkuu Mizengo Pinda kufika
chuoni hapo kusikiliza kilio kinacho wakabili kwa katika Upande wa Afya
kutokana na ungozi ndani ya chuo kushindwa kusikiliza kwa wakati na
kulitolea ufafanuzi wea kudumu.
Wakati
wa maandamano zilikuwa zikisikika sauti na nyimbo zenye shinikizo la
kutaka kiliochao kisikilizwe kwa wakati huku wakiwa wamebeba mabango
yenye ujumbe mbali mbali yakutaka popote alipo waziri mwenye dhamana na
mkuu wake kufika na kusikiliza kile kinacho wakabili katika upande wa
Afya.
Kufuatia mgomo huo ulililazimu jeshi la polisi kufika eneo hilo ili kuweza kutuliza ghasia na mambo mengine ambayo yanaweza kutokea na kuhatarisha hali ya usalama,ambapo jeshi la polisi liliwaamuru weanafunzi hao waliokuwa wakiandamana kutawanyika mara moja katika eneo hilo kabla haijatumika nguvu ya ziada ambayo ingeweza kuchafua hali ya hewa kwa muda mfupui.
Kufuatia mgomo huo ulililazimu jeshi la polisi kufika eneo hilo ili kuweza kutuliza ghasia na mambo mengine ambayo yanaweza kutokea na kuhatarisha hali ya usalama,ambapo jeshi la polisi liliwaamuru weanafunzi hao waliokuwa wakiandamana kutawanyika mara moja katika eneo hilo kabla haijatumika nguvu ya ziada ambayo ingeweza kuchafua hali ya hewa kwa muda mfupui.
Kwa mujibu wa wanafunzi hao, tangu waanze mgomo Aprili 10 mwaka huu, uongozi wa
chuo hicho haujataka kuwasikiliza.
Wakizungumza na TAMBARARE HALISI wanafunzi
wa chuo hicho waliainisha madai takriban saba wakidai ni ya muda mrefu ambayo
hayajapatiwa suluhu.
“Tumegoma kwa sababu kwanza kozi zote za sayansi hazijasajiliwa na bodi husika
na watu waliohitimu wamenyimwa leseni za kazi,” alisema mmoja wa wanafunzi wa
mwaka wa pili wa Shahada ya Famasia,alisema wanalipa ada kubwa ikilinganishwa
na wanafunzi wa mwaka wa kwanza.
“Wanafunzi wa mwaka wa pili na wa tatu wanalipa kuanzia Sh milioni 6.5 hadi Sh milioni tisa na kwa mwaka wa kwanza wanalipa Sh milioni tatu,” alisema mwanafunzi huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake.
“Wanafunzi wa mwaka wa pili na wa tatu wanalipa kuanzia Sh milioni 6.5 hadi Sh milioni tisa na kwa mwaka wa kwanza wanalipa Sh milioni tatu,” alisema mwanafunzi huyo ambaye hakutaka kutaja jina lake.
Madai mengine ya wanafunzi hao ni pamoja na kutokuwa na mtaala unaoeleweka,
uongozi mbovu akiwamo mshauri wa wanafunzi, programu kuchukua miaka mingi
tofauti na vyuo vingine, kushindishwa mitihani kwa makusudi na gharama kubwa ya
kurudia mitihani waliyoshindwa.
Mkurugenzi wa Masoko na Mawasiliano, Kenneth Uki, alikiri kuwapo madai hayo
ingawa mengine si ya kweli,alisema kuhusu kozi kutosajiliwa na bodi husika,
alisema ni kweli Bodi ya Famasia haijasajili kozi za famasia huku ingawa
alisema si kweli kwamba kozi zote za sayansi hazijasajiliwa.
“Tulishapeleka maombi Bodi ya Famasia tangu 2013 na walikuja kufanya ukaguzi awamu ya kwanza na bado hawajarudi kwa awamu ya pili na ya tatu waweze kutupatia usajili,” alisema Uki.
“Tulishapeleka maombi Bodi ya Famasia tangu 2013 na walikuja kufanya ukaguzi awamu ya kwanza na bado hawajarudi kwa awamu ya pili na ya tatu waweze kutupatia usajili,” alisema Uki.
Akizungumzia ada,Uki alisema tayari yamekwisha kupokewa maombi ya wanafunzi
kupunguziwa ada na kwamba kikao cha bodi ya chuo huwa ni mara moja kwa mwaka
hivyo wavute subira.
“Ada ni mkataba kati ya chuo na wanafunzi kwa hiyo linapokuja suala la kutaka
ipungie ni suala la makubaliano baada ya wanafunzi kupeleka maombi yao yanaweza yakakubaliwa au kukataliwa, ” alisema
Uki.
Hata hivyo alisema wanafunzi wanapochagua chuo hawana budi wasome masharti ya
chuo husika ikiwamo ada na kozi zinazotolewa.
Kuhusu madai ya kushindishwa mitihani wanafunzi na gharama kubwa za kurudia
mitihani, alisema wanafunzi wamekuwa watoro na kwamba inahitaji fedha kufanya
maandalizi ya kurudia mitihani.
Msajili wa Baraza la Wafamasia katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,
Elizabeth Shekalaghe amekiri kuwapo maombi ya usajili kutoka KIU akisema bado
zinasubiriwa baadhi ya nyaraka kutoka chuoni hapo.l
“Tulipokea maombi kutoka KIU tukaenda kufanya ukaguzi chuoni hapo na kuwapa masharti na vigezo walivyotakiwa wakamilishe pamoja na kuleta nyaraka, hawakuleta.
“Tulipokea maombi kutoka KIU tukaenda kufanya ukaguzi chuoni hapo na kuwapa masharti na vigezo walivyotakiwa wakamilishe pamoja na kuleta nyaraka, hawakuleta.
“Tukawakumbusha mara mbili Agosti na Septemba mwaka jana bado hawakufanya hivyo
,”alisema Shekalaghe.
Alisema sheria inavitaka vyuo husika visajili kwanza kozi zao na ndipo vifanye
udahili wa wanafunzi na kila baada ya miaka mitatu vinatakiwa kukaguliwa upya.
Migomo
nchini tanzania na kwingineko imekuwa ikifanyika kwa lengo la kutaka
kusikilizwa kwa kile wanachotaka kisikike kutokana na mamlaka husika
kushindwa kulipatia suluhu hivyo kuamua kupaza sauti kwa umoja na
mshikamano ili pengine kila anayesikia huenda akaguswa na hivyo utatuzi
ukapatikana kwa wakati unaostahili.
Licha
ya kuaminika kuwa sauti ya pamoja ionayovuma kwa lengo la kudai haki
kwa maandamano lakini pia sauti hiyo hiyo kama haijatumika vema kwa
misingi ya sheria na kanuni zake huenda ikaleta madhara kama ambayo
yaliyowahi kutokea katika maandamano kadhaa ya watu kuumizwa,kupoteza
masha na hata wengine kubakia na ulemavu wa kudumu katika viungo vya
miili yao.
0 comments:
Post a Comment