Watu 103
kupoteza maisha na watu 138 kujeruhiwa ikiwemo wengine kupata ulemavu wa kudumu
imetokea kwa kipindi cha mwezi mmoja tu katika maeneo mbalimbali hapa
nchini,huku chanzo kikubwa cha ajali hizi zilizopoteza maisha ya watanzania
imedaiwa kusababishwa na uzembe wa baadhi ya madereva.
Jeshi la polisi
kikosi cha usalama barabarani mbali na kubaini vyanzo vya ajali hizo zilizotokea
katika maeneo mbalimbali nchini kwa kutaja kuwa ni uzembe wa baadhi ya madereva,tatizo
la mwendo kasi,ubabe wa baadhi ya madereva kwa magari madogo,mkuu wa kikosi cha
usalama barabarani Mohamed Mpinga,amelazimika kuweka wazi idadi ya vifo
vilivyotokea katika ajali mbalimbali kuanzia mwezi january mwaka huu,ambapo
watu wengi wamepoteza maisha.
Baadhi ya
wanasheria wamesema kuna udhaifu mkubwa katika sheria inayotumika,kwani licha
ya madereva na wamiliki wa mabasi na magari binafsi wakugundulika kusababisha
watu kupoteza maisha kutokana na uzembe wao,hakuna sheria kali inayotumika
kuwabana mbali na kutozwa faini ndogondogo huku ndugu wa marehemu waliopoteza
maisha katika ajali hizo pamoja na majeruhi hasa wale waliachwa na ulemavu wa
kudumu wakibaki njia panda bila kupewa fidia yeyote na wamiliki wa vyombo hivyo.
0 comments:
Post a Comment