Image
Image

Hans Poppe amemtaka Ramadhani Singano ‘Messi’ apeleke kopi ya mkataba.


Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amemtaka kiungo wao, Ramadhani Singano ‘Messi’ apeleke kopi ya mkataba ili kumaliza ubishi.
Hans Poppe amemtaka Singano kufanya hivyo ili kupunguza kelele zinazoendelea sasa.
Singano amekuwa akilalamika kwamba Simba wamecheza mchezo na kumuongezea mwaka mmoja kwenye mkataba wake ulio TFF.
Lakini Hans Poppe amesisitiza mkataba wa Messi unamalizika mwakani na si mwaka huu kama ambavyo amekuwa akisema kiungo huyo.
“Yeye alete mkataba tu, kawaida kunakuwa na kopi tatu. Yake, yetu na ya TFF. Sasa alete yake, sisi tutoe ili kuangalia wapi kuna tatizo.
“Nafikiri haitakuwa busara hili suala kuendelea kukuzwa wakati kulimaliza ni lahisi na mikataba yote ipo,” alisema Hans Poppe.
Hata hivyo, Hans Poppe alisisitiza kwamba anachotakiwa Messi ni kuwasilisha mkataba orijino na si kopi.
"Kopi mtu anaweza kuichezea, hivyo hatutakubali. Alete ule orijino kama ambavyo sisi tutafanya," alisema.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment