Image
Image

News Alert:Kambi rasmi ya upinzani bungeni yaitaka Serikali kutoa muda wa mwisho wa utoaji vitambulisho vya taifa kwa wananchi na kuainisha gharama zilizotumika katika zoezi hilo.

Kambi rasmi ya upinzani Bungeni imeitaka serikali kutoa ukomo wa muda wa ambao wananchi watapatiwa vitambulisho vya taifa na kuainisha gharama zilizotumika katika mchakato mzima wa kutengeneza vitambulisho hivyo pamoja na kutoa taarifa ya idadi ya maghala mapya ya kuhifadhia silaha yaliyojengwa kwa fedha zilizoidhinishwa mwaka wa fedha uliopita ambazo ni sh bilioni 10.

Hayo yamo katika hotuba za wasemaji wa kambi ya upinzani Bungeni wa wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga taifa pamoja na wizara ya mambo ya ndani ya nchi wakati wa kuwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hizo huku baadhi ya wabunge wakishangazwa na kitendo cha wizara ya ulinzi kupangiwa fedha na kushindwa kuzipata.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment