Wizara ya Mambo ya Ndani imesema majeshi ya
usalama yalijibu mapigo kwa kukabiliana na wapiganaji hao katika kijiji cha
Yumbis na kuwatimua , lakini hakukuwa na
taarifa zozote za maafa yaliyotokea.
Mwezi uliopita wapiganaji hao wa al-Shabaab
walivamia Chuo Kikuu cha Garisa na kuua watu wapatao 150 wengi wao wakiwa
wanafunzi.
Katika uvamizi wa hivi karibuni inasemakana
wapiganaji hao waliingia msikiti mmoja wa kijiji hicho na kuhutubia waumini kwa
karibu saa mbili kabla ya kutokomea
porini .
0 comments:
Post a Comment