Image
Image

SERIKALI: Jitihada za kupunguza vifo kutokana na matatizo ya uzazi zimefanyika.


Bunge limeelezwa kuwa kulingana  na takwimu  za Shirika  la Afya Duniani,  Tanzania  haitaweza  kufikia  lengo  namba tano la maendele o  ya Milenia katika kuboresha  afya  ya  uzazi  na hivyo imejipanga kufanikisha lengo hilo ifikapo Mwaka 2020.
Hayo  yamesemwa na Naibu  Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo   JUMA NKAMIA,kwa  niaba ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii  alipokuwa akijibu swali la Mbunge ANASTANZIA WAMBURA aliyetaka  kujua lengo namba tano la Milenia  serikali  imefanikiwa  kwa kiasi gani.
NKAMIA amesema   ni kweli kuwa  lengo  namba  tano  la malengo  ya  maendeleo  ya milenia  ni kupunguza  vifo  vya  wanawake  vinavyotokana    na uzazi  kwa robo tatu  kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2015.
Amesema jitihada  mbalimbali  z imefanyika ili kupunguza  idadi ya wanawake  wanaofariki  dunia kutokana  na matatizo  ya uzazi  ikiwa ni pamoja  na mpango mkakati  wa kuongeza kasi  ya  kupunguza  vifo  vitokanavyo  na uzazi ,watoto wachanga pamoja na  watoto  chini ya miaka  mitano wa mwaka 2008–2015 .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment