Image
Image

Wananchi watakiwa kuwafichua majangili wanaoua tembo na wanyama wengine mkoani Iringa.


Wananchi wanaoishi kuzunguka Hifadhi ya Taifa ya Ruaha mkoani Iringa wametakiwa kushirikiana na hifadhi hiyo kuwafichua majangili wanaoua tembo na wanyama wengine hifadhini humo ili kuzifanya maliasili hizo kuwa endelevu kwa faida ya kizazi hiki na kizazi kijacho

Mkuu wa mkoa wa Iringa Bibi AMINA MASENZA ametoa changamoto hiyo wakati wa makabidhiano ya nyumba mbili za walimu na nyumba moja ya askari polisi katika vijiji vya Kipera na Idodi katika tarafa ya Idodi na Tungamalenga katika tarafa ya Pawaga zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili zilizojengwa kwa ushirikiano wa hifadhi hiyo na wananchi wa tarafa za Idodi na Pawaga na hifadhi hiyo.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha Dakta CHRISTOPHER TIMBUKA amesema mradi wa ujirani mwema umesaidia ujenzi wa miradi mbalimbalimbali ya m aendeleo kwa lengo la kujenga u husiano kati ya hifadhi na wananchi wanaoizunguka .

Naye Ofusa Mtendaji wa kijiji cha Kipera Bwana JOSEPH KALINGA amesema kijiji hicho  kilitumika kama  kama maficho ya majangili waliokuwa wa kiua  tembo katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, lakini kutokana na elimu ya uhifadhi inayotolewa kupitia mradi wa ujirani mwema, wananchi wamebadilika na kushiriki katika shughuli za uhifadhi kwa kuwalinda wanyama wakiwemo tembo wa Ruaha.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment