Baada ya ufafanuzi huo kuhusu habari ambazo simesambazwakatika
mitandao ya kijamii Dr.Magufuli ambaye amepewa na wananchi jina la mzee wa kazi
akaanza ziara yake ya kusaka ridhaa ya watanzania kiongoza Tanzania mkoani Njombe
ambapo amewataka watanzania kupuuza kile kinachoitwa mabadiliko kwa kuwa hata Libya
ilifanya mabadiliko ya kukurupuka kutokana na utamu wa lugha za wapinzani wake
na hii leo wananchi hao wa Libya wanahangaika na kuwataka kumpa fursa ya urais
ili afanye mabadiliko ya kimfumo na kiuchumi taifa lisonge mbele kimaendeleo.
Aidha Dr.Magufuli akizungumza kwa sauti ya kumaanisha kwa
dhati kile anachokisema amewataka watanzania kumwamini kumpa ridhaa ya kuwa
rais na kwamba Tanzania itaendeshwa bila ya ubaguzi na maendeleo ya kweli
yataonekana.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya taifa Mh.Dr.Harrison Mwakyembe
amewaeleza watanzania kuwa Tanzania haitaki viongozi wa maamuzi magumu na
badala yake inamtaka kiongozi mwadilifu atakayesimamia rasilimali za taifa kwa
usawa na haki bila uonevu na ambao wanapaswa kuaminiwa na wakipewa madaraka
hawatadokoa kwa manufaa yao rasilimali za taifa.
Katokana na kile kinachoneka kuwa sera na kampeni za
kistaarabu zinazofanywa na Dr.Magufuli baadhi ya wananchi waliokuwa katika
vyama vya upinzani wamerejesha kadi zao na kujiunga na CCM kwa kile walichodai
ni kuchoshwa kutumika kama ngazi na viongozi wa CHADEMA.
Jumapili ya August 30 ziara za Dr.Magufuli kusaka ridhaa ya
watanzania kuiongoza Tanzania itaendelea mkoani Ruvuma.
0 comments:
Post a Comment