Image
Image

Stewart Hall watolea uvivu wa amuzi.


Licha ya Kocha Mkuu wa Azam,Muingereza, Stewart Hall, kuibuka na ushindi kwenye michezo yake minne mfululizo ya Ligi Kuu Bara, bado amekiri kuwa hafurahishwi na maamuzi yanayotokea kwenye mechi hizo.
Kocha huyo amefunguka kuwa, mara kadhaa amekuwa haridhishwi na waamuzi wa ligi hiyo, lakini ameamua kuweka wazi baada ya maamuzi mabovu zaidi yaliyofanywa kwenye michezo yake miwili ya mwisho dhidi ya Mwadui FC waliyoshinda 1-0 na wa Mbeya City waliyoshinda 2-1.
Stewart alifika mbali na kusema kuwa muda mwingine huwa anafikiria labda waamuzi hawapendi kuona Azam inafanya vizuri, ndiyo maana yanatokea yote hayo na maamuzi yasiyo na haki kwenye mechi zao.
“Waamuzi wamekuwa tatizo sana, kadi nyingi hutolewa hovyo kwenye mechi zetu lakini pia haki imekuwa haipatikani. Ishu si kushinda mechi mfululizo, kinachotakiwa ni mpira wa haki na kuchezesha mechi kwa kufuata sheria na si vinginevyo.
“Kuna muda mtu unaweza kufikiri labda watu hawataki kuona Azam inafanya vizuri kwenye ligi, maana haiwezekani kwenye mechi mbili za mwisho mambo yaende tofauti kabisa, hili si zuri kwa kweli, inabidi tubadilike kwa ajili ya amani na maendeleo ya soka,” alisema Stewart.
Baada ya raundi nne za ligi, Azam inashikilia nafasi ya pili ikiwa na pointi 12, sawa na Mtibwa Sugar walio nafasi ya tatu pamoja na vinara Yanga SC.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment