Image
Image

Latest News:Makinda aweka wazi dhamira ya kuwania Uspika wa Bunge Mwaka huu.


Wakati kasi ikiendelea kwa vigogo ndani ya chama cha Mapinduzi CCM wakipigana vikumbo katika Ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM Lumumba jijini Dar es Salaam kwa kujitokeza kwa wingi kuchukua fomu za kugombea nafasi ya Uspika wa Bunge hatimaye hali imekuwa tofauti kwa aliyekuwa Spika wa Bunge la Kumi la jamhuri ya muungano wa Tanzania Bi.Anne Makinda.

Kutokana na uvumi mwingi ama kile kilichokuwa kikionekana kwamba pengine huenda Bi.Makinda ambaye alikuwa ni Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Bunge la kumi kwamba huenda angewania tena nafasi hiyo kwa kipindi hiki cha uongozi mpya chini wa Dk.Magufuli amesema hana mpango huo kuwania bunge la Kumi na Moja na wala hajathubutu kwenda kuchukua fomu kwani kipindi alichofanya kinatosha.

Hata hivyo baada ya CCM kufungua pazia la watu wanaotaka kuwania nafasi za Uspika na unaibu Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kuchukua fomu hizo ni zaidi ya watu kumi kutoka CCM tayari wamejitokeza.

Katika kujitokeza huko ni pamoja na aliyewahi kuwa waziri wa uchukuzi nchini Tanzania Samuel Sitta ambaye pia aliwahi kuwa Spika wa Bunge la Tisa na Mwaka 2010 alichukua tena fomu hiyo kuwania nafasi hiyo lakini aligonga mwamba baada ya chama hicho kuweka kigezo cha mgombea Mwanamke,hivyo nafasi hiyo kuchukuliwa na Anne Makinda.

Mbali na sita Pia wapo waliochukua fomu akiwemo Dk.Emmanuel Nchimbi,aliwahi kuwa waziri wa mambo ya ndani,Leonce Mulenda,Costa Mahalu aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini italia,Balozi Philip Marmo,Simoni Rubugu,Gosbert  Blandes aliyewahhi kuwa mbunge Karagwe katika bunge lililopita,Didas Masaburi na Dk.Kalokola Muzamili hao wakiwa tu ni baadhi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment