Afisa uhusiano wa hospitali ya
muhimbili bw aminieli eligaeshi amebainisha hayo alipokuwa akipokea msaada wa
vitanda 30 na magodoro yake vya kulaza wagonjwa ambapo amesema suala la
msongamano haliwezi kuepikika hadi majengo yatakapoongezwa kwani idadi ya
wagonjwa inaongezeka kila siku ilihali majengo ni yale yale.
Naye mwakilishi wa mkurugenzi wa
idara ya uuguzi na ubora wa hospitali hiyo bi mariana makanga akizungumza mara
baada ya kupokea msaada huo mbali na kushukuru amesema itawapunguzia wauguzi
adha ya kuhudumia mgonjwa akiwa amelala chini.
Kwa upande wake msamaria aliyetoa
msaada huo amesema ni baada ya rais dk john magufuli kutembelea hospitali hiyo
na kubaini changamoto zinazoikabili hivyo naye akaguswa kusaidia huku akitoa
wito kwa wengine.
Akizungumzia suala la mashine ya
MRI kufanyakazi siku moja baada ya rais kutembelea hospitali hiyo hali iliyozua
maswali mengi kwa wananchi na wagonjwa bw eligaeshi amesema.


0 comments:
Post a Comment