Image
Image

Chelsea washinda, Man Utd walazwa nyumbani.

Chelsea wamerejelea ushindi baada ya kulaza Sunderland 3-1 mechi yao ya kwanza bila Jose Mourinho aliyefutwa Alhamisi.
Uwanjani Old Trafford, mambo yamemwendea mrama meneja Louis van Gaal baada ya vijana wake wa Manchester Utd kukabidhiwa kichapo cha 2-1 na Norwich City.
Kwingineko uwanjani Goodison Park, Leicester wameendelea kushangaza ulimwengu wa soka kwa kukwamilia kileleni EPL kwa kulaza Everton 3-2.
Kufuatia kushindwa Jumamosi, Manchester United sasa wamo nambari tano kwenye jedwali wakiwa na alama 29 sawa na Spurs ambao wamo nambari nne lakini wanawazidi kwa magoli.
United wamo alama tisa nyuma ya Leicester walio kileleni wakiwa na alama 38. Nambari mbili na tatu zinashikiliwa na Arsenal (alama 33) na Manchester City (alama 32), klabu zote mbili zikikutana Jumatatu.
Matokeo kamili yalikuwa kama ifuatavyo:
Chelsea 3-1 Sunderland
Everton 2-3 Leicester
Man Utd 1-2 Norwich
Southampton 0- 2 Tottenham
Stoke 1-2 Crystal Palace
West Brom 1 -2 Bournemouth
19:54 Mechi zinamalizika
19:53 KADI NYEKUNDU kwa West Brom
Salomon Rondon wa West Brom anapewa kadi nyekundu. Sasa wanasalia tisa uwanjani.
19:52 Mechi nyingine inamalizika: Southampton 0-2 Tottenham
19:51 BAOOOO! Everton 2-3 Leicester
Kevin Mirallas anafungia Everton.
19:50 Mechi imemalizika Manchester Utd 1-2 Norwich City
19:49 Manchester United 1-2 Norwich City
Chris Smalling anajaribu bahati kwa kichwa lakini wapi. Mpira wake unaenda nje huku muda ukizidi kuyoyoma.

19:47 Everton 1-3 Leicester
Jamie Vardy anaondoka uwanjani akiwa amejishika paja. Ameumia?


19:44 BAOOO! Stoke 1-2 Crystal Palace
Lee Chung-yong anaweka Palace mbele.
19:43 BAOOO! West Brom 1-2 Bournemouth
Bournebmouth wanapata penalti na kufungiwa na Charlie Daniels.
19:39 BAOOO!West Brom 1-1 Bournemouth
Gareth McAuley anasawazishia West Brom.
19:37 Chelsea 3-1 Sunderland
Loic Remy anaanza kazi mara moja akijipenyeza kulia kisha kutoa kombora ambalo linazuiwa na kipa Costel Pantilimon.
19:36 Chelsea 3-1 Sunderland
Diego Costa anaondolewa uwanjani na nafasi yake anaingia Loic Remy.
19:34 BAOOO! Stoke 1-1 Crystal Palace
Bojan anasawazishia Stoke.
19:33 Manchester United wanaendelea kushambulia vikali Norwich.
19:31 BAOOO! Everton 1-3 Leicester
Leicester wanaendelea kutawala Goodison Park. Shinji Okazaki anawafungia la tatu. Amesaidiwa na Jamie Vardy.
19:28 Chelsea 3-1 Sunderland
Cesc Fabregas anaondolewa uwanjani na badala yake anaingia Jon Obi Mikel
19:25 BAOOO! Everton 1-2 Leicester
Riyad Mahrez anarejesha Leicester mbele kupitia penalti baada ya Tim Howard kumwangusha Jamie Vardy.
19:22 BAOOOO! Manchester United 1-2 Norwich City
Anthony Martial anakomboa moja upande wa Manchester United kwa guu la kushoto.


19:20 Everton 1-1 Leicester
Goodison Park, mshambuliaji Jamie Vardy anapata mpira eneo la hatari, kombora lake linatoka nje.
19:16 Manchester United 0-2 Norwich City
United wanafanya badiliko la kwanza, LVG akimtoa Marouane Fellaini na kuingiza Ander Herrera.
19:15 West Brom 0-1 Bournemouth
Vijana 10 wa West Brom wanafungwa na Adam Smith wa Bournemouth.

19:13 BAOOOO! Chelsea 3-1 Sunderland
Kipa Thibaut Courtois anababaisha kutoka kwa mpira wa kichwa wa Younes Kaboul, na nguvu mpya anatinga bao Fabio Borini.

19:10 BAOOOO! Manchester United 0-2 Norwich City
Alex Tettey anaongezea Norwich la pili Old Trafford.

19:07 BAOOOO! Chelsea 3-0 Sunderland
Oscar anafunga penalti. Mashabiki bado wanaimba jina la Mourinho.
19:05 PENALTI Chelsea 2-0 Sunderland
Chelsea wanapata penalti baada ya Willian kuangushwa na kipa Costel Pantilimon. Alikuwa amepokea pasi kutoka kwa Pedro.
19:01 Chelsea 2-0 Sunderland
Sunderland wamefanya badiliko la pili wakiingiza mshambuliaji Fabio Borini nafasi ya Ola Toivonen.
19:00 Mechi zinaanza tena

18:47 NI WAKATI WA MAPUMZIKO SASA
Chelsea 2 0 Sunderland
Everton 1-1 Leicester
Man Utd 0-1 Norwich
Southampton 0-2 Tottenham
Stoke 0-1 Crystal Palace
West Brom 0-0 Bournemouth

18:47 BAOOO!Stoke 0-1 Crystal Palace
Connor Wickham anafungia Palace kupitia penalti.

18:44 Chelsea 2-0 Sunderland
Uwanjani Stamford Bridge, Chelsea wanaonekana kurejelea makali yao. Wameshambulia sana Sunderland.
18:44 BAOOO!Southampton 0-2 Tottenham
Dele Alli anaongezea Spurs bao la pili.
18:42 Southampton 0-1 Tottenham
Uwanjani St Marys,Harry Kane anaweka Spurs kifua mbele.
18:38 BAOOO! Manchester United 1-0 Norwich City
Cameron Jerome anawapiga chenga walinzi wa Man Utd kisha kumbwaga De Gea.

18:37 KADI NYEKUNDU West Brom 0-0 Bournemouth
West Brom wanasalia 10 uwanjani baada ya James McClean kuonyesha kadi nyekundu.
18:35 Chelsea 2-0 Sunderland
Sunderland nusura wakomboe moja lakini kombora la Duncan Watmore linaelekea nje.

18:32 BAOOOO! Everton 1-1 Leicester
Romelu Lukaku anasawazishia Everton.


18:29 BAOOOO! Everton 0-1 Leicester
Riyad Mahrez anafunga mkwaju wa penalti na kuweka viongozi wa ligi Leicester mbele.
18:28 PENALTI Everton 0-0 Leicester
Ramiro Funes Mori anamwangusha mchezaji wa Leicester down Shinji Okazaki.
18:27 Chelsea 2-0 Sunderland
Meneja wa Sunderland anamtoa Sebastian Coates na kuingiza Adam Johnson.
18:25 Uwanjani Stamford Bridge, Chelsea wanaendelea kutawala. Costa, Oscar na Fabregas wanazomewa na mashabiki kila wanapopata mpira.
18:24 Man Utd wanaendelea kushambulia na kudhibiti mpira Old Trafford. Wanapata kona mbili za haraka lakini hazizai matunda.
18:18 Manchester United wanaendelea kushambulia. Juan Mata anapenya ngome ya Norwich, na kumpitishia mpira Rooney. Rooney anatoa kombora lakini wapi? Man Utd bado hawajafanikiwa kulenga goli.
18:13 BAOOO! Chelsea 2-0 Sunderland
Chelsea wanaongeza la pili kupitia Pedro. Krosi imetoka kwa Branislav Ivanovic upande wa kulia, mpira ukamgonga Sebastian Coates kabla ya kumfikia Pedro.
18:11 Man Utd 0-0 Norwich
Wayne Rooney anatumbukiza mpira wavuni lakini yeye, na mwenzake Marouane Fellaini walikuwa wameotea. Bao linakataliwa.
18:07 BAOOOO! Chelsea 1-0 Sunderland
Branislav Ivanovic, anaifungia Chelsea. Amefunga kwa kichwa baada ya kona kupigwa na Willian.
18:06 Everton 0-0 Leicester
Uwanjani Goodison, Everton wameanza vyema wakishambulia wageni wao, ambao kwa sasa wanaongoza jedwali.
18:03 West Brom 0-0 Bournemouth
Kipa wa West Brom Boaz Myhill anafanyishwa kazi mapema na Junior Stanislas anayetoa kombora kutoka mbali.
18:02 Guus Hiddink ameketi pamoja na Didier Drogba na Roman Abramovich.
Mashabiki wengi wamebeba mabango, wakimuunga mkono Mourinho.

 
18:00 Mechi zinaanza
17:57 Wachezaji wanajiandaa kuingia viwanjani.
Mechi zinazoanza ni:
Chelsea v Sunderland 18:00
Everton v Leicester 18:00
Man Utd v Norwich 18:00
Southampton v Tottenham 18:00
Stoke v Crystal Palace 18:00
West Brom v Bournemouth 18:00
17:52 Meneja mpya wa Chelsea Guus Hiddink yumo Stamford Bridge, sawa na mmiliki wa klabu hiyo Guus Hiddink. Chelsea wanasimamiwa leo na Steve Holland.
17:47 Jose Mourinho, baada ya kufutwa kazi Alhamisi, leo amejitokeza na kwenda kushabikia mechi kati ya Brighton na Middlesbrough katika ligi ya daraja la pili Uingereza, ligi ya Championship katika uwanja wa Amex.
Kabla ya mechi hiyo Middlesbrough inaongoza ligi hiyo, ikifuatwa na Brighton kwa wingi wa mabao, timu zote mbili zikiwa sawa kwa alama 43. Mourinho ni rafiki wa meneja wa Middlesbrough Aitor Karanka.
Middlesbrough mwishowe wamechomoka na ushindi wa 3-0 na kufungua mwanya wa alama tatu kileleni kwa kufikia alama 46.

17:30 Mameneja wametangaza vikosi vyao. Upande wa Manchester United Wayne Rooney amerejea.
Man Utd v Norwich
Man Utd XI: De Gea, Young, Jones, Smalling, Blind, Carrick, Fellaini, Memphis, Mata, Martial, Rooney
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment