Image
Image

Dereva wa basi aliyesababisha ajali na kuua urambo apandishwa Mahakamani.


DEREVA wa basi la Allys Star, Alfa Haji (37) lililokuwa likitokea katika wilaya ya Kaliua kuelekea jijini Mwanza amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Urambo mkoani Tabora, akikabiliwa na mashitaka 22 ikiwemo kusababisha vifo vya watu wanane na majeruhi 13.
Akisoma mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Hassani Momba, Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi Mkaguzi Msaidizi, Felibet Pima alisema kwamba Desemba 15 mwaka huu, saa 12:00 asubuhi katika kijiji cha Vumilia wilaya ya Urambo mtuhumiwa huyo aliendesha gari kizembe na kusababisha vifo vya watu wanane.
Alisema kwamba licha ya kusababisha vifo vya watu wanane pia akiendesha gari kwa uzembe alisababisha majeruhi kwa watu 13. Mwendesha mashitaka huyo aliwataja marehemu waliotambuliwa kuwa ni Hamisi Ramadhani mkazi wa Magili mkoani Tabora, Grace Andrew (24), ambaye ni mkazi wa Ng’ambo Tabora, Paschal Abdul (miezi 8) mkazi wa Bunda,Tipwege Kataga (20), Emeliana Tryphon (24) , Antoni Julius Mkazi wa Wilayani Kaliua, Shija Anton mkazi wa Kaliua na Rahel Mussa Mkazi wa Ulyankulu wilayani Kaliua.
Aidha Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi, Pima aliwataja majeruhi mbele ya Mahakama hiyo kuwa ni Pili Juma (15), Maro Machano (50), Gift Mayunga (29), Ibrahimu Hasani (25), Rahel Mabula (20) Jane Inosent( 29) Anges Michael na Godlifa Alois (35). Wengine ni Santo Lufasiza (28) Mariamu Cosmas (38) Fatuma Juma (19) Yunge Sini (9) na Marthar Luhende (21).
Hata hivyo mtuhumiwa huyo alikana mashitaka yote 22 na amerudishwa rumande baada ya Mahakama kuona ni njia ya kumpatia usalama wake na kesi hiyo itatajwa tena Desemba 31 mwaka huu.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment