Image
Image

Kinacho sababisha umeme kukatika katika maeneo ya jiji la Dar es Salaam chabainika

SHIRIKA la Umeme nchini (Tanesco) limesema tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara hasa nyakati za jioni katika maeneo ya Mbagala, Mtoni Kijichi na Yombo kutokana na mifumo ya umeme katika maeneo hayo kuzidiwa jambo ambalo wameanza kulishughulikia.
Tayari marekebisho katika mifumo ya umeme ya maeneo hayo yameanza na inategemewa tatizo hilo kumalizika kuanzia wiki ijayo. Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Felchesmi Mramba wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo pia alisema, maboresho mengine wanayoyafanya ni pamoja na huduma ya dharura.
Alisema kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi juu ya kuchelewa kushughulikiwa kwa taarifa za hitilafu za umeme na vitengo vya dharura katika maeneo mbalimbali nchini.
“Ili kuondoa kero hii shirika limechukua hatua ambazo zitaanza kutekelezwa kuanzia leo(jana) ambazo ni kuongeza maofisa katika vitengo hivi ili kushughulikia matatizo haya,” alisema Mramba.
Alisema katika kila ofisi ya dharura kutakuwa na Ofisa wa huduma kwa wateja na mhandisi ambao watasimamia muda na ubora wa huduma zinazotolewa kwa wateja wao baada ya kutoa taarifa za dharura.
“Kwa hiyo kuanzia leo (jana) wateja wetu wasije kushangaa wakapigiwa simu na maofisa wetu na kuwauliza kama taarifa zao zimeshughulikiwa, watambue hii ni katika maboresho ya vitengo vya dharura,” alisema.
Naye Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji, Usambazaji Umeme, Sophia Mgonja alisema, bado wanaendelea na maboresho ya kuhakikisha wateja wao wanapata huduma nzuri.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment