Image
Image

Wananchi wajitokeza kumchagua mbunge wa jimbo la Masasi licha ya changamoto kujitokeza.




Wananchi wamejitokeza kwa wingi kupiga kura ya kumchagua mbunge wa jimbo la Masasi licha ya changamoto kadhaa zilizojitokeza ikiwamo ya mawakala wa CUF kukataliwa kwa sababu za kutokidhi vigezo katika mchakato huo.
Baadhi ya wananchi waliofika katika kituo cha kupigia kura cha Msufini one wamesema kitendo hicho kimelenga kuvuruga uchaguzi huo.
Msimamizi msaidizi wa uchaguzi jimbo la Masasi mjini Shaibu Dadi amesema wasimamizi wamelazimika kumkataa na kwamba hatambuliki kisheria kwasabu hana kiapo cha kuwa wakala.
Katika hali isiyo ya kawaida wafuasi wa chama cha wananchi CUF walivamia nyumbani kwa katibu wa UWT kata ya Mkomaindo na kudai kuna masanduku ya kura yamefichwa hali iliyolazimu jeshi la polisi kuzingira nyumba kwa usalama.
Jeshi la polisi limeonekana likivinjari huku na kule kulinda usalama, vyama vinavyogombea nafasi ya umbunge ni CCM, CUF, Chadema, ACT na NLD.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment