Image
Image

Mpango asema hatopenda kuwa waziri ombaomba wa fedha,anaelekeza nguvu kukusanya kodi.

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango amesema kamwe hatapenda kuwa waziri ombaomba wa fedha, bali atahakikisha anaelekeza nguvu katika kukusanya kodi ili nchi iweze kujitosheleza kwa mapato ya ndani.
Aidha, amesema atahakikisha mifumo ya kodi inakuwa rafiki kwa wafanyabiashara na wawekezaji ili wasikimbie kulipa kodi, huku akiahidi kuangalia jinsi ya kuachana na kodi zenye kero kwa Watanzania.
Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati alikabidhi ofisi kwa Kaimu Kamishna Mkuu mpya wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Alphayo Kidata. Kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Fedha wiki iliyopita, Dk Mpango alikuwa Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, wakati Kidata alikuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
“Sipendi kuwa waziri wa kuombaomba hivyo nitaelekeza nguvu zangu katika ukusanyaji kodi na kuona nchi yetu inajitegemea kwa mapato ya ndani kwa kiasi kikubwa, lakini ili kufanya hivyo ni lazima kuziba mianya ya mapato…” alisema Dk Mpango.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment